SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

SUMAJKT Port Services

Hii ni kampuni ya Shirika iliyosajiliwa rasmi mwaka 2020 kwa lengo la kusimamia shughuli za upakiaji na upakuaji wa mizigo bandarini na kuhakikisha usalama wa bidhaa zinazoingia na kutoka nchini. mwaka 2017, ilianza kutoa huduma ya kuratibu na kusimamia wafanyakazi wa kutwa wanaoingia kufanya kazi ndani ya bandari ya Dar es Salaam. 

Mwaka 2019, mradi ulipewa kazi ya kutoa huduma hiyo katika bandari za Kigoma na Mwanza. Kwa sasa, imeingia makubaliano mapya ya kuratibu na kusimamia wafanyakazi katika bandari zote zilizopo chini ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ambazo ni bandari za Dar es Salaam, Mwanza, Tanga, Mtwara, Kigoma, Kyela, Kasanga, Bukoba na Kemondo.

Kampuni inaendelea kufanya kazi kwa weledi na uaminifu katika kutoa huduma na kujenga imani kwa watumiaji wa bandari zote nchini baada ya kuamini kuwa ni sehemu salama ya kupitishia mizigo yao.

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram