Kampuni hii ilisajiliwa mwezi Novemba 2020, ambapo inajishughulisha na uzalishaji wa tofali aina zote (paving, cubestone, fensi louvers) na nguzo za uzio. Ilianza kama mradi mnamo mwaka 1973 ikiwa ni kitengo cha ufundi ujenzi Makao Makuu Lugalo kwa kazi za kutengeneza tofali na kusaga kokoto. Baadae ilihamishiwa JKT eneo la Kunduchi, jijini Dar es Salaam.
Mipango ya baadaye ni kusambaza bidhaa mbalimbali za ujenzi ikiwemo milango, madirisha ya chuma na bidhaa za ‘aluminium’ kwa wateja wanaoihitaji.