SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

Afisa Mtendaji Mkuu

Meja Jenerali Rajabu N Mabele

Mkurugenzi Mtendaji

Kanali Petro Ngata

Karibu SUMAJKT

SUMA JKT Ilianzishwa kwa mujibu wa sheria ya mashirika ya umma ya mwaka 1974 (RE 2002) baada ya amri ya Rais ya mwaka 1982. Nia ya kuanzishwa SUMA JKT ni kusaidia miradi ambayo ina uwezo mkubwa wa uzalishaji ili iweze kuzalisha zaidi na kwa faida na hivyo kuisaidia Serikali katika kupunguza matumizi ya kuendesha shughuli za JKT.

DIRA YA SHIRIKA

“Kuwa Shirika kubwa, lenye sifa kibiashara litakalokuwa na uwezo wa kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) kuendesha shughuli zake”

DHIMA YA SHIRIKA

“Kuanzisha na kuendesha shughuli za uzalishaji mali na huduma kwa tija katika sekta za kilimo, ulinzi, uhandisi na ujenzi, viwanda na biashara na pia kutoa huduma kwa ufanisi, ubora na weledi.”

TUNU/MAADILI YA MSINGI

1. Ubunifu
2. Uadilifu
3. Uwajibikaji
4. Huduma bora kwa wateja
5. Ufanisi
6. Weledi
7. Matokeo chanya

Karibu SUMAJKT

SUMA JKT Ilianzishwa kwa mujibu wa sheria ya mashirika ya umma ya mwaka 1974 (RE 2002) baada ya amri ya Rais ya mwaka 1982. Nia ya kuanzishwa SUMA JKT ni kusaidia miradi ambayo ina uwezo mkubwa wa uzalishaji ili iweze kuzalisha zaidi na kwa faida na hivyo kuisaidia Serikali katika kupunguza matumizi ya kuendesha shughuli za JKT.

DIRA YA SHIRIKA

“Kuwa Shirika kubwa, lenye sifa kibiashara litakalokuwa na uwezo wa kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) kuendesha shughuli zake”

DHIMA YA SHIRIKA

“Kuanzisha na kuendesha shughuli za uzalishaji mali na huduma kwa tija katika sekta za kilimo, ulinzi, uhandisi na ujenzi, viwanda na biashara na pia kutoa huduma kwa ufanisi, ubora na weledi.”

TUNU/MAADILI YA MSINGI

1. Ubunifu
2. Uadilifu
3. Uwajibikaji
4. Huduma bora kwa wateja
5. Ufanisi
6. Weledi
7. Matokeo chanya

HABARI

WAGENI  KUTOKA NCHINI ZIMBABWE WAFURAHISHWA NA UZALISHAJI WA SUMAJKT

Mkufunzi Mkuu kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) nchini Zimbabwe, Kanali Cosmas Kahondera, amesema kuwa wamejifunza na kufurahishwa na Uzalishaji wa bidhaa mbalimbali unaofanywa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT). Kanali Kahondera, amezungumza hayo leo tarehe 04 Julai 2022, alipofanya ziara ya kimafunzo katika kiwanda cha Maji (SUMAJKT BOTTLING CO. LTD) na Nguo (SUMAJKT GARMENT CO. LTD) akiwa pamoja na wakufunzi na wanafunzi wa chuo hicho idadi 28 Mgulani JKT jijini Dar es salaam.
Soma Zaidi

MATUKIO

July 15, 2022

Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa bodi ya SUMAJKT, Meja Jenerali (mstaafu) Farah Mohammed (watatu kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata (watatu kulia)Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT Kanali Shija Lupi (wapili kulia) Mkurugenzi Mwendeshaji SUMAJKT Guard Ltd, Kanali Joseph Masanja (wapili kulia) pamoja na Wakuu wa Miradi Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa jijini Dar es Salaam.

July 4, 2022

Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata , akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika viwanja vya maonesho ya 46 kimataifa ya biashara sabasaba jijini Dar es Salaam.

July 4, 2022

Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika viwanja vya maonesho ya 46 kimataifa ya biashara sabasaba jijini Dar es Salaam.

MATANGAZO

March 5, 2023

JKT Marathon 2023

MIRADI YA SUMAJKT

BAADHI YA WATEJA WETU

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram