SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

Meja Jenerali Rajabu Mabele

Afisa Mtendaji Mkuu (CEO)

Kanali Petro Ngata

Mkurugenzi Mtendaji (ED)

Karibu SUMAJKT

SUMA JKT Ilianzishwa kwa mujibu wa sheria ya mashirika ya umma ya mwaka 1974 (RE 2002) baada ya amri ya Rais ya mwaka 1982. Nia ya kuanzishwa SUMA JKT ni kusaidia miradi ambayo ina uwezo mkubwa wa uzalishaji ili iweze kuzalisha zaidi na kwa faida na hivyo kuisaidia Serikali katika kupunguza matumizi ya kuendesha shughuli za JKT.

DIRA YA SHIRIKA

“Kuwa Shirika kubwa, lenye sifa kibiashara litakalokuwa na uwezo wa kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa(JKT) kuendesha shughuli zake”

DHIMA YA SHIRIKA

“Kuanzisha na kuendesha shughuli za uzalishaji mali na huduma kwa tija katika sekta za kilimo, ulinzi, uhandisi na ujenzi, viwanda na biashara na pia kutoa huduma kwa ufanisi, ubora na weledi.”

TUNU/MAADILI YA MSINGI

1. Ubunifu
2. Uadilifu
3. Uwajibikaji
4. Huduma bora kwa wateja
5. Ufanisi
6. Weledi
7. Matokeo chanya

Karibu SUMAJKT

SUMA JKT Ilianzishwa kwa mujibu wa sheria ya mashirika ya umma ya mwaka 1974 (RE 2002) baada ya amri ya Rais ya mwaka 1982. Nia ya kuanzishwa SUMA JKT ni kusaidia miradi ambayo ina uwezo mkubwa wa uzalishaji ili iweze kuzalisha zaidi na kwa faida na hivyo kuisaidia Serikali katika kupunguza matumizi ya kuendesha shughuli za JKT.

HABARI

WAGENI  KUTOKA NCHINI ZIMBABWE WAFURAHISHWA NA UZALISHAJI WA SUMAJKT

Mkufunzi Mkuu kutoka Chuo cha Ukamanda na Unadhimu (CSC) nchini Zimbabwe, Kanali Cosmas Kahondera, amesema kuwa wamejifunza na kufurahishwa na Uzalishaji wa bidhaa mbalimbali unaofanywa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT). Kanali Kahondera, amezungumza hayo leo tarehe 04 Julai 2022, alipofanya ziara ya kimafunzo katika kiwanda cha Maji (SUMAJKT BOTTLING CO. LTD) na Nguo (SUMAJKT GARMENT CO. LTD) akiwa pamoja na wakufunzi na wanafunzi wa chuo hicho idadi 28 Mgulani JKT jijini Dar es salaam.
Soma Zaidi

MATUKIO

July 11, 2024

Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Gerson Msigwa akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Banda la JKT katika Maonesho ya 48 ya Biashara Kimataifa (Sabasaba) Mkoani Dar es Salaam.

July 6, 2024

Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele(Kushoto) Mkuu wa Tawi la Utawala wa JKT Brigedia Jenerali Hassan Mabena (katikati) na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Petro Ngata wakiangalia samani katika banda la JKT kwenye maonesho ya 48 ya sabasaba

July 3, 2024

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Banda la JKT katika Maonesho ya 48 ya Biashara Kimataifa (Sabasaba) Mkoani Dar es Salaam.

MATANGAZO

  MIRADI YA SUMAJKT  

  Machapisho  

  BAADHI YA WATEJA WETU  

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram