Hii ni kampuni tanzu ya Shirika ambayo inajishughulisha na utoaji huduma za ulinzi. Makao makuu ya kampuni ni Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. Kampuni ilisajiliwa rasmi tarehe 20 Oktoba 2008 na kuanza kazi tarehe 01 Februari 2010 ikiwa na walinzi saba. Kampuni ilizinduliwa rasmi tarehe 28 Machi 2014, na kwa sasa kampuni ina walinzi zaidi ya 14,000 nchi nzima.
Malengo ya kuanzishwa kwa kampuni ni kutoa huduma ya ulinzi kwenye taasisi za Serikali, kampuni za umma na binafsi, kutoa ajira kwa vijana waliohitimu mafunzo ya JKT na mgambo. Pia, kampuni inatoa huduma za ulinzi kwa kutumia teknolojia za kisasa ambazo ni Ulinzi wa Milango (Access Control), Kamera za usalama (CCTV Camera), Mfumo wa ‘alarm’ katika vyombo vya moto, Mfumo wa ‘alarm’ kwa ajili ya kudhibiti moto, uzio wa umeme, Mfumo wa ufuatiliaji magari (Car Tracking System) na Mfumo wa mafuta kwenye vyombo vya moto.
Nyingine ni Mashine ya ukaguzi kwa ajili ya kudhibiti moto, Mashine ya ukaguzi kwa kutumia mionzi, Ufungaji wa simu ya upepo (Radio call), Kufunga na kufungua mlango kwa umeme (Automotive Gates), Ulinzi wa kutumia mbwa na huduma salama ya kusindikiza fedha. Sambamba na huduma hizo kampuni inatoa huduma ya magari ya kubeba wagonjwa na kuzima moto na uokoaji.
Katika kuboresha huduma za ulinzi SUMAJKT Guard Ltd inatoa huduma katika maeneo mbalimbali ya nchi kupitia kanda saba ambazo ni Kanda ya Mashariki, Kanda ya Magharibi, Kanda ya Kusini, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Kanda ya Kati, Kanda ya Ziwa na Kanda ya Kaskazini.