Hapo mwanzo, Shughuli za Uvuvi zilikuwa zikifanyika katika Ziwa Victoria chini ya Kikosi cha Jeshi Rwamkoma (822KJ), kwa upande wa Ziwa Tanganyika chini ya Kikosi cha Jeshi Bulombora (821 KJ) na Bahari ya Hindi chini ya Kkikosi cha Jeshi Mbweni (836KJ). Baadaye, Shirika lilianzisha mradi wa ufugaji wa samaki unaoitwa SUMAPONICS (kwa njia ya kuzungusha maji (Recirculating Aquaculture System) katika Kikosi cha Mbweni JKT mwaka 2017. Mradi huu unazalisha vifaranga vya samaki na kuviuza kwa wahitaji pamoja na kutoa elimu ya ufugaji wa samaki kwa jamii na kuwajengea mifumo ya matenki.