Kutokana na sera ya Serikali kuifanya Tanzania kuwa ya uchumi wa viwanda ifikapo mwaka 2025, Shirika liliitikia wito huo kwa vitendo kwa kuboresha viwanda vilivyopo na kuanzisha viwanda vipya. Kati ya mwaka 2016 hadi 2022 chini ya uongozi wa Maafisa Watendaji Wakuu (CEOs) kwa nyakati tofauti ambao ni Meja Jenerali Michael Isamuhyo, Meja Jenerali Martin Busungu, Meja Jenerali Charles Mbuge na Meja Jenerali Rajabu Mabele ambao wameweza kutekeleza sera hiyo kwa kuimarisha sekta ya viwanda.
Kabla ya kuanzishwa Shirika, shughuli za viwanda vidogovidogo zilikuwa zinafanyika ndani ya Vikosi vya JKT. Miongoni mwa Vikosi 21 Miaka 41 ya SUMAJKT FINALISED.indd 21 27/06/2022 11:32 AMMIAKA 41 YA SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA (SUMAJKT) vya JKT vilivyokuwa vinajihusisha na viwanda ni pamoja na Mgulani ambapo kulikuwa na kiwanda cha ushonaji wa nguo, mahema, useremala, na utengenezaji wa sabuni,, Buhemba kulikuwa na kiwanda cha usokotaji na ufumaji wa vitambaa, Mbweni kulikuwa na kiwanda cha utengenezaji wa mitumbwi, na katika Kikosi cha Ruvu kulikuwa na kiwanda cha ushonaji wa nguo.
Baada ya kuanzishwa kwa Shirika mwaka 1981, miradi hii iliingizwa kwenye Shirika lakini haikufanya vizuri katika soko shindani kutokana na teknolojia duni na uhaba wa mitaji. Shirika katika jitihada za kukabiliana na changamoto za kiteknolojia na uhaba wa mitaji liliingia kwenye biashara ya ubia na makampuni ya nje kati ya Mwaka 2001 mpaka 2013. Makampuni hayo ni Pamoja na TANZASINO, CAMISUMA, CHINA TANZANIA GARMENTS na SUMAJKT ANIT ASFALT. Jitihada hizi za kuboresha sekta ya viwanda ndani ya JKT zilifanywa na Maafisa Watendaji Wakuu (CEOs) waliokuwepo kwa vipindi tofauti ambao ni Meja Jenerali Davis Mwamunyange, Meja Jenerali Abdulrahaman Shimbo, Meja Jenerali Martin Madata, Meja Jenerali Samwel Kitundu, Meja Jenerali Samwel Ndomba na Meja Jenerali Raphael Muhuga.