SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

SUMAJKT Mngeta Plantation (KPL)

Shughuli za uzalishaji kupitia kilimo zinaendeshwa kwenye maeneo mbalimbali ya Makambi na vikosi vya JKT. Kwa sasa, shughuli hizi husimamiwa na mameneja kwenye maeneo husika tofauti na hapo awali ambapo makamanda vikosi walikuwa wakisimamia shughuli hizo. Shirika linaendelea kupanua shughuli za kilimo kwa kutafuta mashamba mapya na yale yanayotolewa na Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina (TR) kwa lengo la kuyaendeleza kibiashara. 

Mwaka 2021, Shirika lilikabidhiwa shamba la ukubwa wa zaidi ya ekari 12,000 lililokuwa likijulikana kama Kilombero Plantation Limited (KPL). Kwa sasa shamba hilo linaitwa SUMAJKT Mngeta Plantation mkoani Morogoro ambako uzalishaji wa mpunga na mahindi kwa kiwango kikubwa unafanyika. Hii ni kutokana na shamba hili kuwa na miundombinu ya kisasa ya kilimo cha umwagiliaji, mashine za kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa na zinazosaidia kuhifadhi mazao ya mpunga na mahindi.

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram