SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

SUMAJKT Leather Products

Kiwanda cha bidhaa za ngozi SUMAJKT Leather Products kipo eneo la Mlalakuwa, jijini Dar es Salaam na kinajishughulisha na utengenezaji wa bidhaa za ngozi kwa ajili ya matumizi ya taasisi za ulinzi, shule, kampuni, pamoja na watu binafsi. Bidhaa zinazozalishwa ni pamoja na viatu, mikanda, mabegi na mikoba. Kiwanda hiki kilianzishwa rasmi tarehe 13 Julai 2017. Aidha, Kiwanda kilianza kwa kutumia moja ya majengo yaliyokuwa Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa Mlalakuwa Dar es Salaam na vyerehani vilivyokuwa vinatumiwa na Kampuni ya CAMISUMA kwa ajili ya uzalishaji wa bidhaa za ngozi. Kwa sasa kiwanda kimefanikiwa kununua vyerehani na mashine za kisasa za kutengeneza bidhaa za aina mbalimbali.
Uzalishaji wa bidhaa za viwandani kwa sasa kwa ajili ya kufanya biashara ni mojawapo ya shughuli kuu ambazo zinaitambulisha Shirika katika tasnia ya Viwanda nchini. Shirika hili limekuwa kichocheo katika uzalishaji, uhamasishaji, na uchangiaji wa bidhaa katika sekta ya viwanda na hivyo kushiriki moja kwa moja katika utoaji wa ajira kwa jamii ya Watanzania sambamba na kukuza uchumi wa viwanda.

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram