SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

SUMAJKT Consultancy Bureau

Kampuni ya Huduma za Ushauri Elekezi katika Majenzi (SCBCL) ni kampuni mpya iliyotokana na uwepo wa wataalamu katika Idara ya Ujenzi NSCD waliokuwa wakijihusisha na usanifu, ukadiriaji majenzi na usimamizi wa miradi ya ujenzi. Wazo la kuanzisha kampuni hii lilitokana na changamoto zilizokuwa zinajitokeza kwa vitengo vya Wasanifu (Architects), Wakadiriaji Majenzi (Quantity Surveyor) na Kampuni ya Uhandisi (Engineering Firms) kushindwa kuomba kazi za ushauri kupitia mwamvuli wa SUMAJKT CCL. Kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Bodi za ERB na AQRB kampuni ya ukandarasi hairuhusiwi kufanya kazi za ushauri hivyo ikaonekana kuna haja ya kuanzisha kampuni inayojitegemea.

SCBCL ilipata usajili wa BRELA mnamo tarehe 21 Mei 2021 na kufanya mabadiliko ya majina ya vitengo mbalimbali ambavyo vimesajiliwa. Vitengo hivyo ni Wasanifu Majengo (Architects), Wakadiriaji Majengo (Quantity Surveyors) na Wahandisi Ushauri (Consulting Engineers). Kampuni inaendelea kufanya kazi na kampuni nyingine na asasi mbalimbali za Serikali na watu binafsi.

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram