SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

SUMAJKT Construction Co. Ltd

Hapo awali, kazi za ujenzi zilianza mwaka 1972 chini ya Brigedi ya Ujenzi (Builders Brigade) iliyokuwa na jukumu la ujenzi wa Makambi ya Jeshi la Kujenga Taifa nchini. Pia ilishiriki katika Ujenzi wa nyumba za kupangisha za Shirika la Nyumba la Taifa (Slum Clearance Scheme) kati ya mwaka 1968 - 1973 kwenye maeneo ya Magomeni na Kinondoni jijini Dar es salaam.

Mwaka1992, “Builders Brigade” ilisajiliwa na Wizara ya Ujenzi na kubadili jina kuwa “National Service Construction Department (NSCD) ambayo ilisajiliwa kuwa Mkandarasi Daraja la Tatu. Mwaka 2004, baada ya kutekeleza kwa ufanisi mradi wa ujenzi wa nyumba 150 za watumishi wa Serikali huko Mbweni, Dar es Salaam, “National Service Construction Department” ilipandishwa daraja “Building Contractor” kutoka daraja la tatu kuwa daraja la kwanza.

 Mwaka 2006 NSCD ilipata Usajili wa Ukandarasi wa Ujenzi wa Barabara Daraja la Nne (Civil Works Contractor Class Four) na Utandazaji Umeme Daraja la Nne (Electrical Contractor Class Four). NSCD imetekeleza kazi za ujenzi nyingi zikiwemo za kitaifa kwa weledi hivyo ilipandishwa madaraja na kupewa daraja la tatu katika “Civil Works Contractor” na daraja la kwanza katika “Electrical Contractor”.
NSCD ilipata usajili wa washauri wataalamu katika fani ya usanifu majengo (Architectural Firm) tarehe 22 Disemba 2017 na kusajiliwa katika kundi la
Wahandisi Washauri (Consulting Engineers) tarehe 19 Aprili 2018. Na mnamo, tarehe 24 Novemba 2018 NSCD ilisajiliwa na BRELA kuwa Kampuni kwa jina la SUMAJKT Construction Company Limited (SCCL).

Kampuni inatekeleza kazi za Ujenzi na Uhandisi kupitia kanda zake saba za Ujenzi ambazo ni Kanda ya Mashariki (Dar es salaam, Pwani na Morogoro), Kanda ya Magharibi (Kigoma, Katavi na Tabora) , Kanda ya Kati (Singida na Dodoma), Kanda ya Kusini (Mtwara, Lindi na Ruvuma), Kanda ya Kaskazini (Kilimanjaro, Tanga, Manyara na Arusha), Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe na Rukwa) na Kanda ya Ziwa (Mwanza, Mara, Kagera, Shinyanga na Geita). 

Kwa pamoja kanda hizi za ujenzi zimefanikisha kutekeleza miradi katika maeneo mbalimbali nchini. Miradi hii ni pamoja na Ujenzi wa nyumba za makazi, Majengo ya ofisi na biashara, Ujenzi wa barabara na madaraja, Ujenzi wa mabwawa ya maji na miundombinu ya maji, Kazi za umeme katika majengo na umeme mkubwa na Kazi za Uhandisi wa Mitambo. Pamoja na kutekeleza miradi ya kibiashara, Shirika hutekeleza pia miradi ya huduma kwa Serikali na jamii kama vile ujenzi wa ukuta unaouzunguka mgodi wa madini ya Tanzanite, Mirerani mkoani Manyara, ujenzi wa majengo mbalimbali ndani ya Ikulu na ukuta unaozunguka Ikulu ya Chamwino, mkoani Dodoma, ujenzi wa jengo la Tume ya Uchaguzi. mkoani Dodoma, Hospitali ya Uhuru, Chamwino mkoani Dodoma na miradi mingine ya Serikali na jamii. Aidha Kampuni imekuwa ikitumia Teknolojia ya kisasa ya Ultimate Building Machine (UBM) katika ujenzi wa baadhi ya majengo ya Serikali na binafsi

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram