SUMAJKT Chang'ombe Furniture Co. Ltd
Kiwanda hiki kilinunuliwa na JKT tangu mwaka 1972 kama kiwanda kidogo cha kuzalisha samani kutoka kwa mmiliki binafsi aitwaye Luige na kukabidhiwa SUMAJKT mwaka 1982 kwa ajili ya mafunzo ya vijana na uzalishaji kibiashara. Baada ya maboresho, kiwanda hiki kilisajiliwa mnamo tarehe 12 Machi 2020 kuwa kampuni kwa jina la “SUMAJKT Chang’ombe Furniture Co. Ltd”. Kiwanda kinachomilikiwa na Shirika kwa asilimia mia moja. Lengo ni kutengeneza samani bora kwa ajili ya taasisi za Serikali, mashirika ya umma, makampuni na watu binafsi.