SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

SUMAJKT Bottling Co. Ltd

Kiwanda hiki kinaozalisha maji ya kunywa yanayoitwa “Uhuru Peak Pure Drinking Water”, kilianzishwa rasmi tarehe 17 Aprili 2018 kwa jina la SUMAJKT Bottling Plant. Kilisajiliwa kuwa Kampuni kwa jina la SUMAJKT Bottling Co. Ltd mwaka 2020. Kiwanda kipo katika eneo la Mgulani JKT jijini Dar es Salaam. Kauli mbiu ya kiwanda ni “The Peak of Natural Purity”.

Wazo la uanzishwaji kiwanda cha maji lilikuja baada ya SUMAJKT kutaka kufufua kiwanda kilichokuwa cha dawa za binadamu cha TANZANSINO kwa kushirikiana na Umoja wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (TSSA). Tathimini ya kitaalamu ilifanywa kwa ushirikiano wa watendaji kutoka SUMAJKT, NHIF na MSD katika eneo la TANZANSINO na kushauri kuwa eneo halikidhi vigezo vya uanzishaji wa kiwanda cha kisasa cha dawa za binadamu. Kwa kuzingatia ushauri huo Shirika liliamua kuanzisha kiwanda cha maji ya kunywa katika eneo hilo.

Maji yanayozalishwa na kiwanda hiki ni sehemu muhimu ya huduma ya maji ya kunywa safi na salama inayotolewa kwa jamii vikiwemo Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Taasisi za Serikali na watu binafsi katika maeneo mbalimbali ya nchi.

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram