SHIRIKA LA UZALISHAJI MALI LA JESHI LA KUJENGA TAIFA
(SUMAJKT)

SUMAJKT Auction Mart

Kampuni hii inajishughulisha na kazi za kukusanya ushuru (Levy Collection), ukusanyaji madeni (Debt Collection) na udalali wa minada (Auctioneers) baada ya kusajiliwa tarehe 11 Juni 2019. Makao Makuu yake yapo Mlalakuwa, jijini Dar es Salaam. Wateja wakubwa wa kampuni hii ni Serikali Kuu, Serikali za Mitaa, Taasisi mbalimbali za kifedha, mashirika madogo madogo ya kifedha na kampuni za biashara. 

Wazo la kuanzishwa SUMAJKT Auction Mart Co. Ltd lilitokana na Shirika kuwa na wateja ambao hawalipi madeni kwa wakati baada ya kupata huduma kutoka kampuni tanzu na hivyo kulazimika kuanzisha kampuni hii badala ya kuendelea kutumia kampuni binafsi kukusanya madeni. Mpaka sasa, kampuni imefanya kazi nyingi hasa kwenye ofisi za halmashauri za wilaya hapa nchini na mpango wa baadaye ni kuboresha huduma zake na kufikia maeneo mengine ya nchi.

Wizara ya Ulinzi

Jeshi la Wananchi la Tanzania

Jeshi la Kujenga Taifa

Shirika La Nyumbu

SUMAJKT© 2023

Imewezeshwa na Kutengenezwa na SUMAJKT

linkedin facebook pinterest youtube rss twitter instagram facebook-blank rss-blank linkedin-blank pinterest youtube twitter instagram