-
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa atuma salamu za Sikukuu kwa kuwatakia Maafisa, Askari, Vijana na watumishi wa umma Heri ya Pasaka.
-
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali, Rajabu Mabele ametuma salamu za Sikukuu za Eid-el-Fitr kwa Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma wote akiwataka washerehekee sikukuu hio kwa utulivu na kiasi.
-
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la kujenga Taifa Brigedia Jenerali Petro Ngata, amepokelewa kwa furaha na Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT katika ukumbi wa Mikutano, Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. Brigedia Jenerali Ngata akipokelewa kwa mara ya kwanza tangu apandishwe cheo hicho kutoka cheo cha Kanali, alianza kukaribishwa kwa gwaride la heshima na baadae kupokelewa na kamati ya Utendaji ya SUMAJKT. Akizungumza katika ukumbi wa mikutano Brigedia Jenerali Ngata ametoa shukrani za dhati kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu Meja Jenerali Rajab Mabele
-
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda amkabidhi tuzo ya Mshidi wa Jumla Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT katika sherehe za kufunga Mashindano ya #cdfcup2024 yaliyofanyika katika Uwanja wa uhuru, jijini Dar es salaam.
-
SUMAJKT yashinda Tuzo ya Mshindi wa Jumla katika Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima (Nane Nane). Tuzo hio imekabidhiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajab Mabele. Meja Jenarali Mabele amesema siri ya ushindi wa JKT katika maonesho mbalimbali nchini ni dhamira ya kufanya kazi kwa bidii na kwa ubunifu mkubwa. Meja Jenerali Mabele ameyasema hayo katika sherehe za Kilele cha Maonesho ya Kilimo ya Kimataifa Nane Nane ambayo kitaifa yameadhimisha Jijini Dodoma na Kufungwa na Mh. Rais wa







