Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali, Rajabu Mabele ametuma salamu za Sikukuu za Eid-el-Fitr kwa Maafisa, Askari na Watumishi wa Umma wote akiwataka washerehekee sikukuu hio kwa utulivu na kiasi.
Similar Posts
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri SUMAJKT aridhishwa na kasi ya ujenzi wa nyumba 5000 Msomera
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri SUMAJKT, Meja Jenerali (mstaafu) Mohamed Farah aridhishwa na kasi ya ujenzi wa nyumba 5000 katika kijiji cha Msomera, wilayani Handeni. Ameyasema hayo wakati alipoongoza wajumbe wa Bodi hio katika ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa nyumba za makazi, unaojengwa na kampuni ya ujenzi ya SUMAJKT, ikiwa ni operesheni chini ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Kufahamu undani wa taarifa hio, tafadhali tazama video hii hapa chini;
Meja Jenerali Farah Mohamed (Mstaafu), aongoza Kikao cha Bodi ya Ushauri ya SUMAJKT
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Meja Jenerali Farah Mohamed (Mstaafu), aongoza Kikao cha Bodi ya Ushauri ya SUMAJKT kupitia utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 kilichofanyika leo tarehe 14 Machi 2025 katika ukumbi wa Mebele jijini Dodoma. Lengo la kikao hicho ni mapitio ya utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2024/2025 pamoja na kupitisha makadirio ya bajeti ijayo ya mwaka wa fedha wa 2025/2026. Kikao hicho cha Bodi ya Ushauri SUMAJKT kimehudhuriwa na Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika Meja Jenerali Rajabu Mabele,…
Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja atembelea SUMAJKT
Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja nchini Comoro Mhe. Mze Mohamed Ibrahim atembelea SUMAJKT akiangalia Bidhaa zinazozalishwa na SUMAJKT. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata alimpokea Gavana wa Ngazidja Mze Mohamed Ibrahim baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), tarehe 05 Octoba 2024. Ambapo Ugeni huo Ulikuja Tanzania kwa ajili ya Mahusiano ya kibiashara na SUMAJKT. Akiambatana na ujumbe kutoka Comoro, Gavana alipata wasaa wa kutembelea na kujionea bidhaa mbalimbali katika Banda la Maonesho ya Bidhaa na Huduma alipotembelea Makao Makuu ya shirika…
WAZIRI WA ULINZI NA JKT AZINDUA BODI MPYA YA SUMAJKT
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb) ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya SUMAJKT kuendeleza mambo mazuri yaliyoanzishwa na Bodi ya shirika hilo iliyomaliza muda wake kwa kuweka mbele Ubunifu, Mikakati pamoja na kuibua Miradi mipya ya kiuwekezaji. Mhe. Waziri Rhimo Nyansaho, amezungumza hayo leo tarehe 14 Januari 2026 baada ya kuzindua Bodi Mpya ya Ushauri ya SUMAJKT katika ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa Chamwino jijini Dodoma. Aidha, Mhe. waziri Nyansaho amewapongeza wajumbe wapya kwa kuteuliwa kwao na kutoa rai kwao kuendelea kusaidia SUMAJKT kusonga mbele na kufikia malengo…
SUMAJKT yatembelewa na Ugeni kutoka Comoros
Ugeni kutoka Kisiwa cha Comoro, tarehe 06 Septemba 23 umetembelea Shirika la uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) lililopo Mlalakua jijini Dar es salaam. Ujumbe huo wa watu watano ukiongozwa na Mhe. Gavana Sitti Farouata Mhoudine umefika Makao Makuu ya SUMAJKT kwa ziara ya kikazi na umepokelewa na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Afisa Mtendaji Mkuu SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele. Mhe. Gavana Sitti Farouata katika ziara hiyo amepata fursa ya kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT kupitia Taarifa fupi iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Utafiti wa SUMAJKT. Luteni Kanali George Wang’ombe.Taarifa hiyo…
Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kuhitimisha Ufungaji wa Mafunzo ya Vijana wa Kujitolea OP Miaka 60 ya Muungano Ruvu JKT
Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kuhitimisha Ufungaji wa Mafunzo ya Vijana wa Kujitolea OP Miaka 60 ya Muungano Ruvu JKT. Mkuu wa Tawi la Mafunzo Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Longinus Nyingo tarehe 16 Aprili 2025 amekagua Maandalizi ya Mwisho kuelekea kuhitimishwa kwa zoezi la Ufungaji wa Mafunzo ya awali ya Kijeshi kwa Vijana wa Kujitolea Operesheni Miaka 60 ya Muungano katika Kikosi cha Ruvu JKT Mlandizi mkoani Pwani. Kanali Nyingo amesema kuwa, zoezi la ufungaji wa Mafunzo katika Vikosi vyote vya JKT lilianza tarehe 8 Aprili 2025 ambapo Mkuu wa JKT alikuwa akiwakilishwa na Wakuu wa Matawi…


