Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa atuma salamu za Sikukuu kwa kuwatakia Maafisa, Askari, Vijana na watumishi wa umma Heri ya Pasaka.
Similar Posts
WANANCHI WA COMORO WAFURAHISHWA NA BIDHAA KUTOKA SUMAJKT
Tarehe 12 hadi 19 mwezi Disemba 2022 kulifanyika Maonyesho ya Kibiashara eneo la ETG Moroni ambapo maonyesho hayo yaliratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro. Katika maonyesho hayo SUMAJKT ilialikwa kwa ujumbe rasmi wa balozi na uwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed. Maonyesho hayo yalikuwa na lengo la kukuza uhusiano wa kiuchumi baina ya serikali na wananchi wa nchi hizo mbili (Tanzania na Comoro) ambapo wananchi Comoro wafurahishwa na bidhaa kutoka SUMAJKT. Wananchi wa Moroni walipata fursa ya kujionea bidhaa mbalimbali zinazozakishwa na SUMAJKT na wengi walionyesha kuridhishwa na viwango vya bidhaa hizo. Katika picha unaweza kushuhudia…
VIJANA WAHITIMU JKT WAASWA MATUMIZI MAZURI YA MITANDAO YA KIJAMII
Mkuu wa Wilaya ya Songea mjini Mhe. Williman Kapenjama, amewaasa na kuwakumbusha vijana wahitimu wa mafunzo ya awali ya kijeshi kundi la Kujitolea Operesheni Miaka 60 ya Muungano juu ya matumizi bora ya mitandao ya kijamii. Vijana wahitimu waaswa matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii. Mhe. Kapenjama, amezungumza hayo leo tarehe 08 Aprili 2025, alipokuwa akifunga mafunzo ya awali ya kijeshi kwa kundi la kujitolea katika kikosi mlale JKT mkoani Ruvuma. Aidha, amebainisha kuwa vijana wengi hawana elimu ya kutosha juu ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii hivyo hutazama mambo ambayo ni kinyume na tamaduni za kiafrika. Nae Mwakilishi…
JESHI la Kujenga Taifa (JKT) latangaza nafasi za kujitolea kwa mwaka 2024 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa vijana wote kutoka Tanzania Bara na Zanzibar
JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limetangaza nafasi za kujitolea kwa mwaka 2024 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa vijana wote kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wenye sifa za kujiunga na Jeshi hilo huku watakaopata nafasi hizo wametakiwa kuripoti katika kambi za JKT kuanzia Novemba 1 hadi 3 Mwaka huu. Akizungumza Septemba 25, 2024 na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa JKT,Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa JKT, Kanali Juma Mrai amesema usaili utaanza Oktoba 1, mwaka huu kupitia Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar. “Mkuu wa Jeshi…
Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT awaasa watendaji juu ya vihatarishi
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, kwa niaba ya Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika Meja Jenerali Rajabu Mabele, amesema, kwa kutambua umuhimu wa udhibiti wa vihatarishi katika utendaji, Shirika limeamua kufanya mafunzo ya usimamizi wa vihatarishi kwa watendaji ili kuwajengea uwezo katika kutambua, kutathimini na kudhibiti vihatarishi kwa lengo la kuleta tija katika utendaji. Brigedia Jenerali Ngata, amezungumza hayo Machi 4, 2026 katika ukumbi wa Umoja unaosimamiwa na SUMAJKT Catering Co.Ltd uliopo Mwenge Dar es Salaam.
Wanafunzi kutoka Nigeria wafurahishwa na shughuli za SUMAJKT
Wanafunzi kutoka Nigeria wafurahishwa na shughuli za SUMAJKT. Ugeni wa Wakufunzi na wanafunzi chuo Cha Taifa Cha Mafunzo ya Usalama nchini Nigeria wafurahishwa na Shughuli za Jeshi la Kunega pamoja na Shirika lake SUMAJKT. Ugeni huo wa Wakufunzi na wanafunzi idadi 25 ukiongozwa na Mkuu wa Msafara huo Makamu Mkuu wa Chuo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Mafunzo Bwana Hyginus Ngele Umepokelewa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Shija Lupi kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele Makao Makuu ya Shirika Mlalakuwa jijini Dar es salaam tarehe…
Waziri wa Ulinzi Angola, aridhishwa na shughuli za SUMAJKT
Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Angola Mhe. Joao Ernesto Dos Santos, ameridhishwa na shughuli zinazofanywa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga (SUMAJKT). Akizungumza baada ya kufanya ziara SUMAJKT leo tarehe 11 Januari 2025, Mhe. Dos Santos, amebainisha kuwa amevutiwa na uzalishaji unaofanywa na Shirika hilo, hivyo wataenda kufanyiakazi nchini kwao. “Wizara yetu ya Ulinzi nchini Angola kupitia Wizara ya Ulinzi na JKT Tanzania tutakuja kusaini hati ya awali ya makubaliano ambayo itaonesha maeneo ya kushirikiana” alisema Mhe. Dos Santos. Aidha, Mhe. Joao Ernesto Dos Santos, ameishukuru Wizara ya Ulinzi na JKT Tanzania kupitia JWTZ kwa kuwezesha…


