Ugeni wa Wakufunzi na Wanafunzi wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa nchini Nigeria (NDC) Wafanya ziara ya Kimasomo Katika Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT)

Ugeni wa Wakufunzi na Wanafunzi wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa nchini Nigeria (NDC) Wafanya ziara ya Kimasomo Katika Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Mlalakuwa Dar es salaam, leo tarehe 04 Machi 2025 kwa lengo la kujifunza namna Shirika linavyofanya Shughuli za Uzalishaji wa Bidhaa hususani Viwandani.

Ugeni huo wa Wakufunzi na wanafunzi idadi 26 ukiongozwa na Mkuu wa Msafara ‘ Air Vice Marshal’ Hanidu Ibrahim, umepokelewa na Kaimu Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Shija Lupi, kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika Meja Jenerali Rajabu Mabele.

Akizungumza baada ya Ziara hiyo, ‘Air Vice Marshal’ Ibrahim amebainisha wamehamasika na uzalishaji unaofanywa na SUMAJKT kupitia kiwanda cha Taa, Maji, Ushonaji Nguo na Bidhaa za Ngozi.

“Lengo la ziara yetu ni Kujifunza Shughuli zinazofanywa na Jeshi la Kujenga Taifa na Shirika lake SUMAJKT na namna linavyochangia katika Uchumi wa Tanzania, hivyo tumejifunza Mengi tutaenda kuyatumia katika Kujenga Uchumi wa Taifa letu Nigeria” amesema.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, Kanali Shija Lupi amesema Ugeni huo umeridhishwa na kazi za SUMAJKT.

Ugeni huo umepata fursa ya kutembelea Kiwanda cha Taa (SUMAJKT Skyzon Co.Ltd), Kiwanda cha Maji (SUMAJKT Bottling Co.Ltd), Kiwanda cha Ushonaji Nguo (SUMAJKT Garments Co.Ltd) na Bidhaa za Ngozi.

Similar Posts

  • Waziri wa Ulinzi Angola, aridhishwa na shughuli za SUMAJKT

    Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Angola Mhe. Joao Ernesto Dos Santos, ameridhishwa na shughuli zinazofanywa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga (SUMAJKT). Akizungumza baada ya kufanya ziara SUMAJKT leo tarehe 11 Januari 2025, Mhe. Dos Santos, amebainisha kuwa amevutiwa na uzalishaji unaofanywa na Shirika hilo, hivyo wataenda kufanyiakazi nchini kwao. “Wizara yetu ya Ulinzi nchini Angola kupitia Wizara ya Ulinzi na JKT Tanzania tutakuja kusaini hati ya awali ya makubaliano ambayo itaonesha maeneo ya kushirikiana” alisema Mhe. Dos Santos. Aidha, Mhe. Joao Ernesto Dos Santos, ameishukuru Wizara ya Ulinzi na JKT Tanzania kupitia JWTZ kwa kuwezesha…

  • |

    Dkt. Rhimo Nyansaho atembelea SUMAJKT MM

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho (MB) leo tarehe 22, Julai 2026, ametembelea Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) kwa lengo la kujionea shughuli za uzalishaji na maendeleo yanayotekelezwa na shirika hilo. Katika ziara hiyo, Mhe. Waziri Nyansaho, alipata maelezo kuhusu miradi mbalimbali ya uzalishaji mali, mafanikio yaliyopatikana pamoja na mipango ya kuimarisha uwezo wa shirika katika kuchangia maendeleo ya taifa. Aidha, ziara hiyo ilihitimishwa kwa Mhe. Waziri Nyansaho, kutembelea kiwanda cha Maji ya Kunywa ya Uhuru Peak (SUMAJKT Bottling Co.Ltd) na Kiwanda cha Ushonaji nguo (SUMAJKT Garments Co….

  • SUMAJKT yatembelewa na Ugeni kutoka Comoros

    Ugeni kutoka Kisiwa cha Comoro, tarehe 06 Septemba 23 umetembelea Shirika la uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) lililopo Mlalakua jijini Dar es salaam. Ujumbe huo wa watu watano ukiongozwa na Mhe. Gavana Sitti Farouata Mhoudine umefika Makao Makuu ya SUMAJKT kwa ziara ya kikazi na umepokelewa na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Afisa Mtendaji Mkuu SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele. Mhe. Gavana Sitti Farouata katika ziara hiyo amepata fursa ya kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT kupitia Taarifa fupi iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Utafiti wa SUMAJKT. Luteni Kanali George Wang’ombe.Taarifa hiyo…

  • MKUU WA JKT AISHUKURU SERIKALI KULIWEZESHA JKT KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE

    Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa kutekeleza majukumu yake Meja Jenerali Mabele ametoa shukrani hizo tarehe 16 Januari 2025 Makao Makuu ya JKT wakati wa hafla ya uzinduzi wa Magari aina ya Isuzu D Max Pick Up idadi tisa (9) kwaajili ya Matumizi ya shughuli za kiutawala ndani ya Jeshi la Kujenga Taifa. Magari hayo yamekabidhiwa kwa baadhi ya Wakurugenzi wa Makao Makuu ya JKT na Makamanda Vikosi vya Jeshi la Kujenga Taifa.

  • DED SUMAJKT atembelea Mafinga.

    DED SUMAJKT atembelea Mafinga. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Shija Sahani Lupi ametembelea Miradi mbalimbali inayoendeshwa na Shirika hilo katika Halimashauri ya mji mdogo Mafinga Mkoani Iringa. Tukio hilo limejiri tarehe 17 Oktoba 2025 mara baada ya kushiriki Mahafali ya 29 ya kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Kawawa JKT akiwa Mgeni rasmi. Brigedia Jenerali Lupi ametembelea Majengo ya madarasa mapya yatakayotumika kujifunza kwa njia ya mtandao (E-learning), shule ya Awali na Msingi, eneo la shamba jipya la mifugo (Ng’ombe) na baada ya kutembelea maeneo hayo alipata fursa ya kuongea…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *