Similar Posts
JESHI la Kujenga Taifa (JKT) latangaza nafasi za kujitolea kwa mwaka 2024 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa vijana wote kutoka Tanzania Bara na Zanzibar
JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limetangaza nafasi za kujitolea kwa mwaka 2024 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa vijana wote kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wenye sifa za kujiunga na Jeshi hilo huku watakaopata nafasi hizo wametakiwa kuripoti katika kambi za JKT kuanzia Novemba 1 hadi 3 Mwaka huu. Akizungumza Septemba 25, 2024 na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa JKT,Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa JKT, Kanali Juma Mrai amesema usaili utaanza Oktoba 1, mwaka huu kupitia Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar. “Mkuu wa Jeshi…
DKT. STERGOMENA TAX AONGOZA ZOEZI LA UPANDAJI MITI ENEO LA MAKAO MAKUU YA ULINZI WA TAIFA KIKOMBO DODOMA
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 31 Januari 2025, amewaongoza Maafisa, Askari, Vijana na Watumishi wa Umma katika zoezi la upandaji miti katika eneo la Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa Kikombo pamoja na eneo la viwanja vya makazi ya watumishi wa Wizara ya Ulinzi na JKT, Chinangali 2 nje kidogo ya Jiji la Dodoma. Akizungumza wakati wa zoezi hilo la upandaji miti, Mhe. Dkt. Stergomena Tax, amesema zoezi hilo ni muendelezo wa kuunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt Samia…
Mej Jen. Isamuhyo (Mstaafu) aongoza kikao cha bodi SUMAJKT
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Meja Jenerali Michael Isamuhyo (mstaafu) ameongoza Kikao cha Bodi ya Ushauri SUMAJKT na kufanya ziara ya kutembelea Viwanda vya Shirika ambavyo ni kiwanda cha Viatu na Bidhaa Ngozi, Kiwanda cha Insignia, Kiwanda cha Maji, Kiwanda cha Ushonaji pamoja na kituo cha mafuta SUMAJKT Energies. Ziara hiyo ya Bodi ya Ushauri SUMAJKT kutembelea viwanda imefanyika Machi 5, 2026 jijini Dar es Salaam. Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya utambulisho wa shughuli zinazofanywa na Shirika kwa Bodi ya Ushauri Mpya iliyoanza kufanya kikao cha kwanza leo…
MKUU WA JKT AISHUKURU SERIKALI KULIWEZESHA JKT KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa kutekeleza majukumu yake Meja Jenerali Mabele ametoa shukrani hizo tarehe 16 Januari 2025 Makao Makuu ya JKT wakati wa hafla ya uzinduzi wa Magari aina ya Isuzu D Max Pick Up idadi tisa (9) kwaajili ya Matumizi ya shughuli za kiutawala ndani ya Jeshi la Kujenga Taifa. Magari hayo yamekabidhiwa kwa baadhi ya Wakurugenzi wa Makao Makuu ya JKT na Makamanda Vikosi vya Jeshi la Kujenga Taifa.
SUMAJKT Kutafuta Fursa za Biashara visiwani Comoro
Ujumbe wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) unazuru nchini Comoro kwa minajili ya utafutaji wa fursa za ushirikiano wa kibiashara ikiwa ni siku chache baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Wenyeviti na Watendaji Wakuu ambao ulihimiza Mashirika ya Umma kuangazia fursa nje ya nchi. Ziara hiyo inafuatia mwaliko wa Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja Mheshimiwa Ibrahim Mze na inataratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro inaongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Petro Ngata. Mara baada ya kuwasili, Ujumbe wa SUMA JKT ulipata fursa ya kufanya mazungumzo na Gavana wa Kisiwa cha…
BRIGEDIA JENERALI NGATA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAFANYABIASHARA NCHINI COMORO
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi ka Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata amefanya mazungumzo na Jumuiya ya wafanyabiashara kisiwani Comoro katika ukumbi wa Chambre de Commerce Ngazidja uliopo kisiwani humo. Kikao hicho kimefanyika tarehe 5 Septemba 2024, na wafanyabiashara wanaochukua bidhaa Tanzania na kuzipeleka nchini Comoro, Brigedia Jenerali Ngata alipata fursa ya kueleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT hususani katika Sekta ya Ujenzi, Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata ameeleza nia thabiti ya SUMAJKT kuhitaji kufanya kazi na wafanyabiashara hao katika nyanja ya Ujenzi na Kilimo. Kwa upande wa wafanyabiashara kisiwani Comoro wamesema…


