Similar Posts
Waziri Kabudi aridhishwa na Ujenzi wa viwanja kwa ajili ya CHAN.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Palamagamba Kabudi (Mb) ameridhishwa na kazi inayofanywa na Kampuni ya SUMAJKT Construction Company Ltd, katika ujenzi wa viwanja vya mazoezi kwa ajili michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa Ndani (CHAN) yatakayofanyika mwezi Februari mwaka 2025. Katika Ukaguzi huo Profesa Kabudi, amefafanua kwamba viwanja hivyo vitakamilika ifikapo tarehe 21 Januari 2025 kwa ajili ya kuanza kutumika kwa mazoezi ya michuano ya CHAN. Nae Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, kwa niaba JWTZ ameeleza kwamba JKT limekabidhiwa kazi hivyo litaitekeleza kazi hiyo kwa muda uliopangwa….
Wataalamu wa Utafiti na Ushauri wa Kilimo kutoka Kampuni ya CAMPO nchini Brazil wametembelea Shamba la SUMAJKT Mngeta Plantation
Wataalamu wa Utafiti na Ushauri wa Kilimo kutoka Kampuni ya CAMPO nchini Brazil wametembelea Shamba la SUMAJKT Mngeta Plantation lililopo Halmashauri ya Mlimba mkoani Morogoro kuanzia tarehe 11 Februari 2025. Wawakilishi wa kampuni ya CAMPO ambao ni Prof Jamil Macedo ambaye ni Mtalaam wa Udongo pamoja na Bwana Cezar Rizzi Mtalaam wa Umwagiliaji wamewasili Nchini Tanzania Tarehe 10 Februari 2025 na kupokelewa na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata, Kisha ugeni huo kuelekea Morogoro kutembelea Shamba ambalo awali liliitwa Kilombero Plantation Company Limited (KPL) na sasa SUMAJKT Mngeta Plantation kwa lengo la kufanya utafiti na kutoa ushauri wa…
DED SUMAJKT atembelea Mafinga.
DED SUMAJKT atembelea Mafinga. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Shija Sahani Lupi ametembelea Miradi mbalimbali inayoendeshwa na Shirika hilo katika Halimashauri ya mji mdogo Mafinga Mkoani Iringa. Tukio hilo limejiri tarehe 17 Oktoba 2025 mara baada ya kushiriki Mahafali ya 29 ya kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Kawawa JKT akiwa Mgeni rasmi. Brigedia Jenerali Lupi ametembelea Majengo ya madarasa mapya yatakayotumika kujifunza kwa njia ya mtandao (E-learning), shule ya Awali na Msingi, eneo la shamba jipya la mifugo (Ng’ombe) na baada ya kutembelea maeneo hayo alipata fursa ya kuongea…
Waziri wa Ulinzi Angola, aridhishwa na shughuli za SUMAJKT
Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Angola Mhe. Joao Ernesto Dos Santos, ameridhishwa na shughuli zinazofanywa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga (SUMAJKT). Akizungumza baada ya kufanya ziara SUMAJKT leo tarehe 11 Januari 2025, Mhe. Dos Santos, amebainisha kuwa amevutiwa na uzalishaji unaofanywa na Shirika hilo, hivyo wataenda kufanyiakazi nchini kwao. “Wizara yetu ya Ulinzi nchini Angola kupitia Wizara ya Ulinzi na JKT Tanzania tutakuja kusaini hati ya awali ya makubaliano ambayo itaonesha maeneo ya kushirikiana” alisema Mhe. Dos Santos. Aidha, Mhe. Joao Ernesto Dos Santos, ameishukuru Wizara ya Ulinzi na JKT Tanzania kupitia JWTZ kwa kuwezesha…
RC CHALAMILA AAGIZA HALMASHAURI ZIFUNGE TAA ZA SUMAJKT
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Albert Chalamila ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zilizopo Dar es Salaam kuhakikisha wanafika kiwanda cha SUMAJKT Skyzone kilichopo Mlalakua jijini hapo ili kutoa oda za kutengeneza taa bora za barabarani. “Tumepita tumeona teknolojia ya kiwanda hiki., naomba nitoe neno rasmi.., wakurugenzi wote wa halmashauri za Dar es Salaam, kufanya ziara mara moja katika kiwanda hiki, na ikiwezekana kutoa oda za taa.., ili ziweze kufungwa kwenye mji wetu kuhakikisha mji unafanya kazi masaa 24.” Naye Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata amesema kwamba Kiwanda hiko ni cha kwanza kabisa kwa aina…
JESHI la Kujenga Taifa (JKT) latangaza nafasi za kujitolea kwa mwaka 2024 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa vijana wote kutoka Tanzania Bara na Zanzibar
JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limetangaza nafasi za kujitolea kwa mwaka 2024 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa vijana wote kutoka Tanzania Bara na Zanzibar wenye sifa za kujiunga na Jeshi hilo huku watakaopata nafasi hizo wametakiwa kuripoti katika kambi za JKT kuanzia Novemba 1 hadi 3 Mwaka huu. Akizungumza Septemba 25, 2024 na Waandishi wa Habari Makao Makuu ya JKT Chamwino Mkoani Dodoma kwa niaba ya Mkuu wa JKT,Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala Jeshi la Kujenga Taifa JKT, Kanali Juma Mrai amesema usaili utaanza Oktoba 1, mwaka huu kupitia Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar. “Mkuu wa Jeshi…


