-
-
SUMAJKT yatembelewa na Ugeni kutoka Comoros
Ugeni kutoka Kisiwa cha Comoro, tarehe 06 Septemba 23 umetembelea Shirika la uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) lililopo Mlalakua jijini Dar es salaam. Ujumbe huo wa watu watano ukiongozwa na Mhe. Gavana Sitti Farouata Mhoudine umefika Makao Makuu ya SUMAJKT kwa ziara ya kikazi na umepokelewa na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) na Afisa Mtendaji Mkuu SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele. Mhe. Gavana Sitti Farouata katika ziara hiyo amepata fursa ya kuona shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT kupitia Taarifa fupi iliyowasilishwa na Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Utafiti wa SUMAJKT. Luteni Kanali George Wang’ombe.Taarifa hiyo…
-
Waziri Bashungwa atembelea shamba la SUMAJKT Mngeta mkoani Morogoro
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh. Innocent Bashungwa akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Kilombero Mh. Dunstan Kyobya tarehe 8.03.2023 amefanya ziara katika shamba la SUMAJKT MNGETA PLANTATION . Shamba hilo linasimamiwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) lililopo katika tarafa ya Mngeta kijiji cha Itongowa Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro. Akiongea baada ya kukagua shamba hilo na miundombinu yake Mhe. Bashungwa amesema shamba haya kwa muda mrefu lilikaa bila matumizi yeyote baada ya mwekezaji kusitisha shughuli za kilimo. Kwa hiyo ikampendeza Mh. Rais na Amiri Jeshi Mkuu shamba hilo likabidhiwe kwa matumizi…
-
SUMAJKT Electric Co Ltd kuwasha umeme vijiji 51 wilayani Kishapu, Shinyanga.
Zoezi la uzinduzi wa kuwasha umeme limefanyika Februari 17, 2023 wilayani Kishapu, katika Kijiji cha Itilima Shule ya Msingi Isunda, mkoani Shinyanga huku vijiji vitatu vikiwashiwa pia huduma ya umeme ambavyo ni Itilima, Ikonokelo na Ipeja. Mkandarasi SUMAJKT Electric Co Ltd ambaye anatekeleza mradi wa Nishati Vijijini (REA) awamu ya tatu mzunguko wa Pili wilayani Kishapu na Shinyanga, ameanzakusambaza huduma za umeme katika Vijiji, Kaya na Taasisi za Serikali. Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akizungumza wakati wa uzinduzi wa kuwasha umeme wilayani Kishapu kwa vijiji hivyo vitatu, amepongeza kasi ambayo SUMAJKT Electric Co Ltd wameanza nayo ya kusambaza…
-
WATANZANIA WANUFAIKA NA FURSA ZINAZOTOLEWA NA SUMAJKT
Tarehe 16 Januari 2023, Mkuu wa tawi la utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena alizindua magari 17 kwa ajili ya kuimarisha a utendaji wenye tija na kuboresha huduma za ulinzi. Aidha aliendelea kusema kwamba SUMAJKT itaendelea kutengeneza fursa mbalimbali kupitia kampuni ya SUMAJKT na hivyo kunufaisha Watanzania kwa ujumla. Bregedia Jenerali Hassan Mabena liendelea kuwashukuru na kuwaasa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kuendelea kufanyakazi kwa kupitia kampuni tanzu za SUMAJKT.


