Similar Posts
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa atuma salamu za Sikukuu
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa atuma salamu za Sikukuu kwa kuwatakia Maafisa, Askari, Vijana na watumishi wa umma Heri ya Pasaka.
RUVU JKT WAACHANA NA MATUMIZI YA KUNI NA MKAA
Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax ameupongeza uongozi wa kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mkoani Pwani kwa kuachana na matumizi ya nishati ya kuni na mkaa na kuanza kutumia nishati ya gesi kwa asilimia 100. Ruvu JKT waachana na matumizi ya kuni na mkaa. Mhe.Dkt. Tax ametoa pongezi hizo tarehe 3 Aprili 2025 wakati alipofanya ziara kikosini hapo na kujionea namna kikosi hicho chini ya Uongozi wa kamanda kikosi Kanali Peter Mnyani unavyotekeleza kwa vitendo maelekezo ya serikali ya kuachana na matumizi ya kuni na mkaa kwa Taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100. Amepongeza ubunifu wa…
Wakufunzi CUJKT watembelea SUMAJKT
Wakufunzi CUJKT watembelea SUMAJKT. Wakufunzi na Maafisa wanaoshiriki Kozi Elekezi kutoka Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Taifa (CUJKT) tarehe 18 Machi 2025 wamefanya Ziara ya kimasomo katika Shirika la Uzalishaji la Jeshi la kujenga Taifa (SUMAJKT) kwa lengo la kuona Shughuli zinazofanywa na Kampuni zake Tanzu zilizopo eneo la Makao Makuu ya Shirika hilo Mlalakuwa na zilizopo Mwenge jijini Dar es Salaam. Ziara hiyo iliyolenga kujifunza kuhusu shughuli zinazofanywa na SUMAJKT, namna ambavyo huratibiwa na kutekelezwa pamoja na mchango wa Shirika kwa JKT na taifa kwa Ujumla, itaendelea hapo kesho tarehe 19 machi 2025 ambapo Wakufunzi na wanafunzi…
Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta
Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amesema shirika lina dhamira ya kuendelea kujitanua na kuimarisha miundombinu ya kimkakati ya biashara ikiwemo sekta ya nishati. Brigedia Jenerali Petro Ngata, amesema hayo katika uzinduzi wa gari la kusafirishia mafuta la Kampuni ya SUMAJKT Logistiki leo tarehe 26 Mei 2025, Makao Makuu ya Shirika Mlalakuwa Dar es salaam. Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata, amefafanua gari hilo litaongeza ufanisi katika usambazaji wa nishati ya…
DED SUMAJKT atembelea Mafinga.
DED SUMAJKT atembelea Mafinga. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Shija Sahani Lupi ametembelea Miradi mbalimbali inayoendeshwa na Shirika hilo katika Halimashauri ya mji mdogo Mafinga Mkoani Iringa. Tukio hilo limejiri tarehe 17 Oktoba 2025 mara baada ya kushiriki Mahafali ya 29 ya kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Kawawa JKT akiwa Mgeni rasmi. Brigedia Jenerali Lupi ametembelea Majengo ya madarasa mapya yatakayotumika kujifunza kwa njia ya mtandao (E-learning), shule ya Awali na Msingi, eneo la shamba jipya la mifugo (Ng’ombe) na baada ya kutembelea maeneo hayo alipata fursa ya kuongea…
Serikali yalikabidhi SUMAJKT ujenzi wa viwanja vitano vya michezo
Serikali kwa kupitia Wizara ya Michezo na Utamaduni imelikabidhi Shirika la Uzalishaji Mali za Jeshi la kujenga Taifa (SUMAJKT) Ujenzi wa Viwanja vya michezo idadi vitano. Makabidhiano hayo yamefanyika katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT amesema ujenzi wa viwanja hivyo utafanyika katika mtindo wa Operesheni ili kuhakikisha mradi unakamilika ndani ya Muda uliowekwa. Taarifa zaidi, tizama video hii hapa chini:


