Mnadhimu Mkuu afunga kikao cha Wakuu wa Viwanda

Mnadhimu Mkuu afunga kikao cha Wakuu wa Viwanda. Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Luteni Jenerali Salum Haji Othman, amefunga Kikao cha Wakuu wa Viwanda na Mashirika ya Kijeshi ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki leo tarehe 26 Feb 2025  katika hoteli ya Girrafe jijini Dar es Salaam.

Luteni Jenerali Salum Othman, amesema Mkutano huo huibua fursa, Masoko  na namna nzuri ya kuboresha teknolojia  ya Viwanda na Mashirika ya jumuiya hiyo. Mnadhimu Mkuu afunga kikao cha Wakuu wa Viwanda.

Akizungumza kuhusu lengo la Mkutano huo, ameeleza ni kuweka pamoja  na kuimarisha ushirikiano wa Mashirika na Viwanda vinavyomilikiwa  na Majeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi Kikao cha Wakuu wa Viwanda na Mashirika ya Kijeshi ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ambaye ni Mkuu wa Shirika la Nyumbu Brigedia Jenerali Seif Hamis, amesema kikao hicho hufanyika  nchi moja hadi nyingine ambapo  kwa mwaka huu kimefanyika Tanzania na mwakani kitafanyika nchini Rwanda.

Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Kanali Shija Lupi, akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata, amesema Wakuu wa Mashirika  na Viwanda wa Jumuiya hiyo  wamevutiwa na bidhaa zinazozalishwa  na Jeshi la Ulinzi Tanzania. Mnadhimu Mkuu afunga kikao cha Wakuu wa Viwanda.

Awali kabla ya Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Luteni Jenerali Salumu Haji Othman, kufunga mkutano wajumbe walitembelea Kiwanda cha Taa cha SUMAJKT Skyzon Co. Ltd na Maonesho maalumu ya bidhaa za Viwanda vya Mashirika ya Jeshi la Ulinzi Tanzania ambayo ni  SUMAJKT, MZINGA na NYUMBU katika viwanja vya TPDF Lugalo Golf Club.

Mkutano huo ambao ni wa watatu kufanyika pamoja na maonesho tangu kuanzishwa kwake unalenga kuonesha fursa zilizopo kwa kila nchi mwanachama katika eneo la malighafi, vipuri na bidhaa zilizokamilika ili ziweze kupata Masoko ndani ya ukunda kwa nchi wanachama wa kabla ya kuziuza nje ya ukanda na mabara mengine ili kujipatia kipato na kujijengea uchumi tegemevu.

Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube

Similar Posts

  • |

    RC CHALAMILA AAGIZA HALMASHAURI ZIFUNGE TAA ZA SUMAJKT

    Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Albert Chalamila ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zilizopo Dar es Salaam kuhakikisha wanafika kiwanda cha SUMAJKT Skyzone kilichopo Mlalakua jijini hapo ili kutoa oda za kutengeneza taa bora za barabarani. “Tumepita tumeona teknolojia ya kiwanda hiki., naomba nitoe neno rasmi.., wakurugenzi wote wa halmashauri za Dar es Salaam, kufanya ziara mara moja katika kiwanda hiki, na ikiwezekana kutoa oda za taa.., ili ziweze kufungwa kwenye mji wetu kuhakikisha mji unafanya kazi masaa 24.” Naye Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata amesema kwamba Kiwanda hiko ni cha kwanza kabisa kwa aina…

  • |

    KAMISHNA WA JKT KUTOKA NCHINI NAMIBIA ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA SUMAJKT

    Kamishna wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini Namibia Dkt. Felix Masukubili amefanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), Leo tarehe 18 Novemba 2024 Mlalakuwa Jijini Dar es Salaam. Dkt. Masukubili amepokelewa na Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji Kanali Festus Mang’wela. Akiwa katika ziara hiyo amejionea shughuli za uzalishaji Mali zinazofanywa na SUMAJKT ikiwemo kiwanda cha kutengeneza Taa cha SUMAJKT SKYZONE CO.LTD ambacho kinazalisha taa zinazotumia nishati ya jua na umeme, kilichopo Mlalakuwa…

  • |

    Brigedia Ngata azindua magari ya Usafi SUMAJKT

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amezindua magari matano yenye thamani zaidi ya shilingi Bilioni moja ya Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa (SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co.Ltd) Kwa niaba ya Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele. Akizindua magari hayo Leo tarehe 19 Novemba 2024, Brigedia Jenerali Petro Ngata ameeleza kuwa Menejimenti ya SUMAJKT imejiwekea mikakati ya kuendelea kuongeza vitendeakazi ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake. Nae Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa ya SUMAJKT, Kapteni Rosemary…

  • |

    BRIGEDIA JENERALI NGATA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAFANYABIASHARA NCHINI COMORO

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi ka Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata amefanya mazungumzo na Jumuiya ya wafanyabiashara kisiwani Comoro katika ukumbi wa Chambre de Commerce Ngazidja uliopo kisiwani humo. Kikao hicho kimefanyika tarehe 5 Septemba 2024, na wafanyabiashara wanaochukua bidhaa Tanzania na kuzipeleka nchini Comoro, Brigedia Jenerali Ngata alipata fursa ya kueleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT hususani katika Sekta ya Ujenzi, Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata ameeleza nia thabiti ya SUMAJKT kuhitaji kufanya kazi na wafanyabiashara hao katika nyanja ya Ujenzi na Kilimo. Kwa upande wa wafanyabiashara kisiwani Comoro wamesema…

  • |

    Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi

    Naibu Waziri Mambo ya Ndani Mhe. Daniel Sillo ayashauri mashirika ya Kijeshi ndani ya Nchi wanachama katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutumia Sayansi na Teknolojia katika uzalizalishaji wa bidhaa zao. Mhe. Sillo amesema hayo leo tarehe 25 Februari 2025 alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Mashirika yanayo milikiwa na  Majeshi ya  nchi za  Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika hoteli ya Geraffe iliyopo jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi, Amefafanua kuwa Mkutano huo hufanyika kila mwaka ili kutathmini utendaji kazi wa Mashirika na Viwanda vilivyopo ndani ya Majeshi yaliyopo katika Jumuiya ya…

  • | | |

    WANANCHI WA COMORO WAFURAHISHWA NA BIDHAA KUTOKA SUMAJKT

    Tarehe 12 hadi 19 mwezi Disemba 2022 kulifanyika Maonyesho ya Kibiashara eneo la ETG Moroni ambapo maonyesho hayo yaliratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro. Katika maonyesho hayo SUMAJKT ilialikwa kwa ujumbe rasmi wa balozi na uwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed. Maonyesho hayo yalikuwa na lengo la kukuza uhusiano wa kiuchumi baina ya serikali na wananchi wa nchi hizo mbili (Tanzania na Comoro) ambapo wananchi Comoro wafurahishwa na bidhaa kutoka SUMAJKT. Wananchi wa Moroni walipata fursa ya kujionea bidhaa mbalimbali zinazozakishwa na SUMAJKT na wengi walionyesha kuridhishwa na viwango vya bidhaa hizo. Katika picha unaweza kushuhudia…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *