|

MAAFISA FANYENI KAZI KWA BIDII, MJIIMARISHE KIUTENDAJI – MEJA JENERALI ( MSTAAFU) MADAWILI

Meja Jenerali (Mstaafu) Zawadi Madawili ametoa wito kwa Maafisa wanawake wa Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania kufanya kazi kwa bidii ili kujiimarisha kiutendaji katika nafasi zao mbalimbali wanazohudumu.

Meja Jenerali Mstaafu Madawili ameyasema hayo tarehe 02 Mei 2025 katika kikao cha Umoja wa Maafisa wa kike wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wanaofanyia kazi Jeshi la Kujenga (JKT) pamoja na Kamandi nyingine ambacho kimefanyika katika Hoteli ya Ndege Beach Mbweni JKT Jijini Dar es salaam.

Aidha ameeleza siri ya kudumu muda mrefu katika Utumishi ni kufuata Misingi iliyowekwa ambayo ni pamoja na Nidhamu katika kazi, roho ya kupendana, Ushirikiano na Moyo wa kujituma kwa Maslahi ya Jeshi na Taifa kwa Ujumla.

Naye Mkuu wa Tawi la Logistiki na Uhandisi Jeshini ambaye ni Mlezi na mmoja wa Waasisi wa Umoja huo Meja Jenerali Hawa Kodi amesema Lengo la kuanzisha Kundi lilikuwa ni Kuweka Umoja na Mshikamano kwa Maafisa wanawake katika kusaidiana kwenye nyakati mbalimbali wakati na baada ya Utumishi.

Kwa Upande wake Mwenyekiti wa Umoja huo Meja Ester Ryoba Amesema dhumuni la kikao ni kuwakumbusha Maafisa wanawake Majukumu yao Kijeshi pamoja na Kijamii kuendana na Nafasi walizonazo sambamba na kuwahimiza Kuhusu Shughuli za JKT zikiwemo kulea vijana na Uzalishaji Mali.

Maafisa hao wanawake sambamba na kushiriki kikao hicho pia wametembelea Vivutio vya Utaalii vilivyopo Mbweni JKT ambavyo ni Mbweni JKT Zoo, Mandhari ya Ndege Beach Hotel pamoja na kutembela Maeneo ya Fukwe ya Bahari ya Hindi inayopakana na kikosi hicho cha Jeshi.

Viongozi wengine walioudhuria Kikao hicho ni pamoja na Meja Jenerali Grace Mwakipunda (Mstaafu), Meja Jenerali Lilian Kingazi (Mstaafu), Brigedia Jenerali Sara Rwambali ( Mstaafu), Brigedia Jenerali Janeth Izengo, Brigedia Jenerali Solotina Nshushi, Maafisa Wakuu na Maafisa Wadogo

Umoja huo wa Maafisa wanawake Unajumuisha Maafisa wanaofanyia kazi JKT na ambao waliwahi kuhudumu JKT kwa sasa wamehamia katika Kamandi nyingine za Jeshi Ulinzi la wananchi wa Tanzania.

Similar Posts

  • |

    Brigedia Ngata azindua magari ya Usafi SUMAJKT

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amezindua magari matano yenye thamani zaidi ya shilingi Bilioni moja ya Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa (SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co.Ltd) Kwa niaba ya Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele. Akizindua magari hayo Leo tarehe 19 Novemba 2024, Brigedia Jenerali Petro Ngata ameeleza kuwa Menejimenti ya SUMAJKT imejiwekea mikakati ya kuendelea kuongeza vitendeakazi ili kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yake. Nae Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa ya SUMAJKT, Kapteni Rosemary…

  • Marehemu Meja Jenerali Busungu azikwa Luchelele Mwanza

    Waziri Wa Ulinzi na Jeshi La Kujenga Taifa Mhe. Stargomena Lawrence Tax, ameongoza Maafisa, Askari, Vijana, Watumishi wa Umma na Waombolezaji katika Mazishi ya Mwili Wa Marehemu Meja Jenerali Martin Busungu (Mstaafu) yaliyofanyika katika Kijiji Cha Luchelele Jijini Mwanza tarehe 28 Desemba 2024. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda, katika Mazishi hayo Mkuu wa Jeshi La Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, amesema Marehemu Meja Jenerali Busungu (Mstaafu) enzi za uhai wake akiwa mtumishi ndani ya Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania ametumikia Jeshi kwa kipindi…

  • SUMAJKT Yatwaa tuzo Sabasaba

    SUMAJKT Yatwaa tuzo Sabasaba. Jeshi la Kujenga Taifa kupitia Shirika lake la Uzalishaji Mali (SUMAJKT) limeibuka mshindi wa Kwanza katika Samani na Ubunifu wa ndani katika Maonyesho ya 49 ya Biashara Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dara es Salaam. Tuzo ya Ushindi huo imekabidhiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Tanzania Mhe. Selemani Jafo, kwa Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, katika ufunguzi wa Maonesho hayo leo tarehe 7 Julai 2025 katika Viwanja vya Sababa jijini Dar es Salaam. Akizungumzia Ushindi huo Mkuu wa JKT…

  • Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa aongoza waombolezaji kumuaga Meja Jenerali Charles Mbuge

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 16 Octoba, 2024 katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo, jijini Dar es Salaam ameongoza Maafisa, Askari, Watumishi wa Umma pamoja na waomboleazaji, kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Charles Mbuge, aliyefariki Dunia tarehe 12 Octoba 2024. Miongoni mwa viongozi walioungana na Waziri wa Ulinzi na JKT kumuaga na kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Jenerali Mbuge, ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Albert Chalamila, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda, Mnadhimu…

  • SUMAJKT yazindua gari kuongeza ufanisi shule ya Kawawa

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amezindua Gari aina ya TATA Marcopolo kwa ajili ya Matumizi ya Shule ya Awali na Msingi ya Kawawa iliyopo Wilaya ya Mafinga Mkoani Iringa. Akizungumza mara baada ya Uzinduzi huo Brigedia Jenerali Ngata ameutaka Uongozi wa Shule hiyo kutunza Vitendea kazi vinavyo nunuliwa ikiwemo gari hilo ili viweze kufanya kazi kwa Muda mrefu kwa manufaa ya Shule na Shirika kwa Ujumla. Akitoa taarifa fupi kabla ya Uzinduzi huo Mkuu wa Shule ya Kawawa Kanali Ernest Sikaponda amelishukuru shirika kwa kufanikisha Ununuzi wa gari…

  • Brigedia Jenerali Petro Ngata apokelewa kwa Furaha SUMAJKT

    Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la kujenga Taifa Brigedia Jenerali Petro Ngata, amepokelewa kwa furaha na Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT katika ukumbi wa Mikutano, Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. Brigedia Jenerali Ngata akipokelewa kwa mara ya kwanza tangu apandishwe cheo hicho kutoka cheo cha Kanali, alianza kukaribishwa kwa gwaride la heshima na baadae kupokelewa na kamati ya Utendaji ya SUMAJKT. Akizungumza katika ukumbi wa mikutano Brigedia Jenerali Ngata ametoa shukrani za dhati kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu Meja Jenerali Rajab Mabele…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *