Usajili wa SUMAJKT MARATHON, Sunday 7 June 2026 UMEFUNGULIWA RASMI na CEO wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa kushirikiana na CRDB Bank.
JISAJILI KUPITIA TOVUTI YA www.sumajktmarathon.co.tz
Twendezetu Pace ya Kwata
Mapigano Na Mwendo
Usajili wa SUMAJKT MARATHON, Sunday 7 June 2026 UMEFUNGULIWA RASMI na CEO wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa kushirikiana na CRDB Bank.
JISAJILI KUPITIA TOVUTI YA www.sumajktmarathon.co.tz
Twendezetu Pace ya Kwata
Mapigano Na Mwendo
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri SUMAJKT, Meja Jenerali (mstaafu) Mohamed Farah aridhishwa na kasi ya ujenzi wa nyumba 5000 katika kijiji cha Msomera, wilayani Handeni. Ameyasema hayo wakati alipoongoza wajumbe wa Bodi hio katika ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa nyumba za makazi, unaojengwa na kampuni ya ujenzi ya SUMAJKT, ikiwa ni operesheni chini ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Kufahamu undani wa taarifa hio, tafadhali tazama video hii hapa chini;
Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) limeweka malengo ya kufikika na linaendelea kusimamia miradi kwa ufanisi ili kuleta tija kwa shirika. Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya (SUMAJKT) Meja Jenerali (mstaafu) Farah Mohamed, amesema hayo tarehe 19 Oktoba 2024 katika kikao cha kwanza cha malengo ya shirika cha mwaka wa fedha ujao wa 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa SUMAJKT Tower uliopo jijini Dodoma. Kikao hicho kilihudhuriwa wajumbe wa Bodi akiwemo Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata pamoja na wajumbe waalikwa…
” KUSITISHWA KWA MAFUNZO YA JKT KULILETA ATHARI KUBWA IKIWEMO YA MMOMONYOKO WA MAADILI”Wakuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (Wastaafu)Meja Jenerali Martin Madata (Mstaafu) na Meja Jenerali Samwel Kitundu (Mstaafu), wakielezea umuhimu wa Mafunzo ya JKT, athari zilizopatikana baada ya kusitishwa kwa Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria na Kujitolea pamoja na Mafanikio yaliyopatikana Baada ya kurejeshwa kwa Mafunzo hayo. Wameyasema hayo wakati wa Mahojiano Maalumu ya Mafanikio yaliyopatikana ndani ya JKT kwa kipindi cha Miaka 60 ya Uwepo wake nchini.https://www.instagram.com/reel/DGvnVdetkhE/?igsh=ZmJua2s1NWlvcndw Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube
Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa ya SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co. Ltd imetia Saini Mkataba wa kufanya Usafi katika Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Katika Maeneo ya Soko la Buguruni Pamoja na Soko la Ilala leo tarehe18 Februari 2025. Hafla hiyo ambayo imehudhuriwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Elihuruma Mabelya, Mstahiki Meya wa Jiji Mhe. Omary Kumbilamoto, Madiwani, na wadau wa Maendeleo imehusisha pia Uzinduzi wa Magari yaliyo nunuliwa na jiji yatakayotumika Katika Usafi. Akizungumza mara baada ya Kutia Saini Mkataba huo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Jonas Mpogolo,…
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleza mafunzo ya vijana wa JKT. Mkuu wa JKT amshukuru Rais na Amiri Jeshi Mkuu mafunzo ya JKT. Meja Jenerali Mabele, ameyasema hayo leo tarehe 17 Aprili 2025 alipokuwa anahitimisha mafunzo ya Awali ya kijeshi kwa vijana wa Operesheni miaka 60 ya Muungano katika kikosi Cha Ruvu JKT kilichopo mlandizi mkoani Pwani. Amesema Malezi ni suala Mtambuka, yanaanzia ngazi ya familia, Vijana wanapofika makambini….
Timu ya Mpira wa Miguu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa SUMAJKT, imewasili Jijini Tanga hi tarehe 10 Novemba 2024, kwa ajili ya kushiriki Michuano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma Tanzania (SHIMMUTA) iliyoanza Kutimua vumbi katika jiji hilo. Akizungumza mara baada ya kuwasili Jijini Tanga Katibu wa Kamati ya SHIMMUTA Kapteni Kichawele Bokassa, amesema timu imejiandaa vizuri kushiriki Michuano hiyo.