Similar Posts
Mej Jen. Isamuhyo (Mstaafu) aongoza kikao cha bodi SUMAJKT
Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Meja Jenerali Michael Isamuhyo (mstaafu) ameongoza Kikao cha Bodi ya Ushauri SUMAJKT na kufanya ziara ya kutembelea Viwanda vya Shirika ambavyo ni kiwanda cha Viatu na Bidhaa Ngozi, Kiwanda cha Insignia, Kiwanda cha Maji, Kiwanda cha Ushonaji pamoja na kituo cha mafuta SUMAJKT Energies. Ziara hiyo ya Bodi ya Ushauri SUMAJKT kutembelea viwanda imefanyika Machi 5, 2026 jijini Dar es Salaam. Aidha, ziara hiyo ni sehemu ya utambulisho wa shughuli zinazofanywa na Shirika kwa Bodi ya Ushauri Mpya iliyoanza kufanya kikao cha kwanza leo…
WAZIRI WA ULINZI NA JKT AZINDUA BODI MPYA YA SUMAJKT
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb) ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya SUMAJKT kuendeleza mambo mazuri yaliyoanzishwa na Bodi ya shirika hilo iliyomaliza muda wake kwa kuweka mbele Ubunifu, Mikakati pamoja na kuibua Miradi mipya ya kiuwekezaji. Mhe. Waziri Rhimo Nyansaho, amezungumza hayo leo tarehe 14 Januari 2026 baada ya kuzindua Bodi Mpya ya Ushauri ya SUMAJKT katika ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa Chamwino jijini Dodoma. Aidha, Mhe. waziri Nyansaho amewapongeza wajumbe wapya kwa kuteuliwa kwao na kutoa rai kwao kuendelea kusaidia SUMAJKT kusonga mbele na kufikia malengo…
RC CHALAMILA AAGIZA HALMASHAURI ZIFUNGE TAA ZA SUMAJKT
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Albert Chalamila ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zilizopo Dar es Salaam kuhakikisha wanafika kiwanda cha SUMAJKT Skyzone kilichopo Mlalakua jijini hapo ili kutoa oda za kutengeneza taa bora za barabarani. “Tumepita tumeona teknolojia ya kiwanda hiki., naomba nitoe neno rasmi.., wakurugenzi wote wa halmashauri za Dar es Salaam, kufanya ziara mara moja katika kiwanda hiki, na ikiwezekana kutoa oda za taa.., ili ziweze kufungwa kwenye mji wetu kuhakikisha mji unafanya kazi masaa 24.” Naye Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata amesema kwamba Kiwanda hiko ni cha kwanza kabisa kwa aina…
Shule ya Jitegemee JKT yatimiza miaka 50, Jenerali Mhona atia neno
Mkuu wa Tawi la Mafunzo na Oparesheni Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania JWTZ Meja Jenerali Ibrahim Michael Muhona ameipongeza Shule ya Sekondari Jitegemee JKT kwa kutimiza Miaka 50 Tangu kuanzishwa kwake. Akizungumza katika Sherehe ya Maadhimisho hayo zilizoambatana na Harambee maalaumu ya kuchangia maboresho ya Shule hiyo Meja Jenerali Muhona amesema JWTZ linaunga mkono dhamira ya Mageuzi inayofanyika, huku akitoa wito kwa walimu kuhakikisha Shule inaendeleza viwango bora vya Ufahulu. Kilele cha maadhimisho ya Miaka 50 ya Jitegemee JKT kilifanyika tarehe 01 Novemba 2024 ukumbi wa Isamuhyo Mgulani JKT. CHANGIA ELIMU KWA MABORESHO YA MIUNDO MBINU1.NMB….236100419222.CRDB…01508929587003.LIPA….22426113 TIGO.4.LIPA….54359412 VODACOMMajina…
Mkurugenzi SUMAJKT awataka Watendaji kutumia fursa
Mkurugenzi SUMAJKT awataka Watendaji kutumia fursa. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata amewataka Wakurugenzi Waendeshaji, Wakuu wa Shule na Miradi kutumia vizuri fursa zilizopo katika maeneo yao ya kazi ili kuongeza tija kwa Shirika. Brigedia Jenerali Ngata ameyasema hayo tarehe 15 Agosti 2025 katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT (KUS) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika kikao hicho Brigedia Jenerali Ngata amehimiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo ya Shirika. Aidha, amewasisitiza kuendelea kuzalisha Bidhaa na kutoa huduma katika…
WATANZANIA WANUFAIKA NA FURSA ZINAZOTOLEWA NA SUMAJKT
Tarehe 16 Januari 2023, Mkuu wa tawi la utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena alizindua magari 17 kwa ajili ya kuimarisha a utendaji wenye tija na kuboresha huduma za ulinzi. Aidha aliendelea kusema kwamba SUMAJKT itaendelea kutengeneza fursa mbalimbali kupitia kampuni ya SUMAJKT na hivyo kunufaisha Watanzania kwa ujumla. Bregedia Jenerali Hassan Mabena liendelea kuwashukuru na kuwaasa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kuendelea kufanyakazi kwa kupitia kampuni tanzu za SUMAJKT.


