Similar Posts
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa atuma salamu za Sikukuu
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa atuma salamu za Sikukuu kwa kuwatakia Maafisa, Askari, Vijana na watumishi wa umma Heri ya Pasaka.
MAAFISA JKT WAMEASWA KUTEKELEZA KWA WELEDI JUKUMU LA MALEZI YA VIJANA
Maafsa JKT wameaswa kutekeleza kwa weledi jukumu la malezi ya vijana. Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Kanali Juma Mrai amewaasa Maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanaofanyia kazi Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kutekeleza kwa weledi jukumu la Malezi ya Vijana. Kanali Mrai ametoa rai hiyo tarehe 21 Machi 2025 wakati akihitimisha Semina Elekezi ya Maafisa wa JWTZ waliopewa Uhamisho kwenda JKT, iliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Taifa (CUJKT) kilichopo Kimbiji Jijini Dar es Salaam Jeshi la Kujenga Taifa limekuwa likiendesha Semina Elekezi kwa watendaji wake ili kuwajengea uwezo wa…
SUMAJKT yazindua gari kuongeza ufanisi shule ya Kawawa
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amezindua Gari aina ya TATA Marcopolo kwa ajili ya Matumizi ya Shule ya Awali na Msingi ya Kawawa iliyopo Wilaya ya Mafinga Mkoani Iringa. Akizungumza mara baada ya Uzinduzi huo Brigedia Jenerali Ngata ameutaka Uongozi wa Shule hiyo kutunza Vitendea kazi vinavyo nunuliwa ikiwemo gari hilo ili viweze kufanya kazi kwa Muda mrefu kwa manufaa ya Shule na Shirika kwa Ujumla. Akitoa taarifa fupi kabla ya Uzinduzi huo Mkuu wa Shule ya Kawawa Kanali Ernest Sikaponda amelishukuru shirika kwa kufanikisha Ununuzi wa gari…
Brigedia Jenerali Petro Ngata Ameitaka Kampuni ya Umeme ya SUMAJKT Electric Co Ltd kuvitunza vitendea kazi
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), Brigedia Jenerali Petro Ngata Ameitaka Kampuni ya Umeme ya SUMAJKT Electric Co Ltd kuvitunza vitendea kazi vinavyonunuliwa ili viweze kudumu na kuleta tija kwa Shirika. Amezungumza hayo Tarehe 14 Februari 2025, baada ya kufanya Uzinduzi wa Gari Jipya la utawala lililonunuliwa na Kampuni hiyo kwa lengo la kuongeza ufanisi. Awali akitoa taarifa fupi ya ununuzi wa gari hilo Mkurugenzi Mwendeshaji wa SUMAJKT Electric Co Ltd. Meja James Mhame, amesema kuongezeka kwa gari hilo kutarahisisha utekelezaji wa majukumu yao. SUMAJKT Electric Co.Ltd Inajishughulisha na Kandarasi mbalimbali za Miundombinu…
Timu ya Mpira wa Miguu SUMAJKT yawasili Tanga kushiriki SHIMMUTA
Timu ya Mpira wa Miguu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa SUMAJKT, imewasili Jijini Tanga hi tarehe 10 Novemba 2024, kwa ajili ya kushiriki Michuano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma Tanzania (SHIMMUTA) iliyoanza Kutimua vumbi katika jiji hilo. Akizungumza mara baada ya kuwasili Jijini Tanga Katibu wa Kamati ya SHIMMUTA Kapteni Kichawele Bokassa, amesema timu imejiandaa vizuri kushiriki Michuano hiyo.
SUMAJKT LAJIWEKEA MALENGO MWAKA WA FEDHA 2024/’25
Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) limeweka malengo ya kufikika na linaendelea kusimamia miradi kwa ufanisi ili kuleta tija kwa shirika. Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya (SUMAJKT) Meja Jenerali (mstaafu) Farah Mohamed, amesema hayo tarehe 19 Oktoba 2024 katika kikao cha kwanza cha malengo ya shirika cha mwaka wa fedha ujao wa 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa SUMAJKT Tower uliopo jijini Dodoma. Kikao hicho kilihudhuriwa wajumbe wa Bodi akiwemo Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata pamoja na wajumbe waalikwa…


