Mwenyekiti kamati ya NaneNane akaribisha wananchi Dodoma. Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Wakulima Nanenane Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Shija Lupi amewakaribisha wananchi wote hapa nchini kutembelea Maonesho ya Wakulima Nanenane Kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni Dodoma na Kikanda katika Kanda zote ambazo Jeshi hilo linashiriki.
Similar Posts
DED SUMAJKT atembelea Mafinga.
DED SUMAJKT atembelea Mafinga. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Shija Sahani Lupi ametembelea Miradi mbalimbali inayoendeshwa na Shirika hilo katika Halimashauri ya mji mdogo Mafinga Mkoani Iringa. Tukio hilo limejiri tarehe 17 Oktoba 2025 mara baada ya kushiriki Mahafali ya 29 ya kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Kawawa JKT akiwa Mgeni rasmi. Brigedia Jenerali Lupi ametembelea Majengo ya madarasa mapya yatakayotumika kujifunza kwa njia ya mtandao (E-learning), shule ya Awali na Msingi, eneo la shamba jipya la mifugo (Ng’ombe) na baada ya kutembelea maeneo hayo alipata fursa ya kuongea…
Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja atembelea SUMAJKT
Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja nchini Comoro Mhe. Mze Mohamed Ibrahim atembelea SUMAJKT akiangalia Bidhaa zinazozalishwa na SUMAJKT. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata alimpokea Gavana wa Ngazidja Mze Mohamed Ibrahim baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), tarehe 05 Octoba 2024. Ambapo Ugeni huo Ulikuja Tanzania kwa ajili ya Mahusiano ya kibiashara na SUMAJKT. Akiambatana na ujumbe kutoka Comoro, Gavana alipata wasaa wa kutembelea na kujionea bidhaa mbalimbali katika Banda la Maonesho ya Bidhaa na Huduma alipotembelea Makao Makuu ya shirika…
GAVANA WA COMORO AVUTIWA NA BIDHAA ZA SUMAJKT
Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja nchini Comoro Mhe. Mze Mohamed Ibrahim, ameridhishwa na Huduma na Bidhaa zinazozalishwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT). Mhe. Mze Ibrahim amebainisha hayo baada ya ziara yake Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es salaam ambayo imelenga kuendeleza Uhusiano wa kibiashara baina ya SUMAJKT na nchi ya Comoro. Katika ziara hiyo Gavana ameambatana na Wakurugenzi wa Chemba ya Biashara kutoka nchini humo, Pamoja na Mwakilishi wa Balozi wa Comoro nchini Tanzania. Baada ya kuwasili Makao Makuu ya SUMAJKT Mhe.Mze Mohammed amepatiwa taarifa kuhusu SUMAJKT ambayo imeainisha maeneo ambayo wanaweza kushirikiana…
SUMAJKT WAINGIA MAKUBALIANO NA VISIWA VYA COMORO, MEJA JENERALI MABELE ANENA “TUNAWAJENGEA BARABARA”
Habari zaidi tazama video hii hapa chini..
Waziri wa Ulinzi Angola apongeza malezi ya JKT kwa vijana
Waziri wa Ulinzi wa Angola apongeza namna Jeshi la Kujenga Taifa linavyowalea Vijana wa Kitanzania. Waziri wa Ulinzi wa Angola Mhe.Joao Ernesto Das Santos ametoa pongezi hizo katika mwendelezo wa ziara yake hapa nchini, ambapo ametembelea Kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mkoa wa Pwani tarehe 9 Januari 2025.
Timu ya Mpira wa Miguu SUMAJKT yawasili Tanga kushiriki SHIMMUTA
Timu ya Mpira wa Miguu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa SUMAJKT, imewasili Jijini Tanga hi tarehe 10 Novemba 2024, kwa ajili ya kushiriki Michuano ya Shirikisho la Michezo la Mashirika ya Umma Tanzania (SHIMMUTA) iliyoanza Kutimua vumbi katika jiji hilo. Akizungumza mara baada ya kuwasili Jijini Tanga Katibu wa Kamati ya SHIMMUTA Kapteni Kichawele Bokassa, amesema timu imejiandaa vizuri kushiriki Michuano hiyo.


