Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja atembelea SUMAJKT

Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja nchini Comoro Mhe. Mze Mohamed Ibrahim atembelea SUMAJKT akiangalia Bidhaa zinazozalishwa na SUMAJKT.

Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata akimpokea Gavana wa Ngazidja, Mze Mohamed Ibrahim alipowasili Makao Makuu ya SUMAJKT.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata alimpokea Gavana wa Ngazidja Mze Mohamed Ibrahim baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), tarehe 05 Octoba 2024. Ambapo Ugeni huo Ulikuja Tanzania kwa ajili ya Mahusiano ya kibiashara na SUMAJKT.

Akiambatana na ujumbe kutoka Comoro, Gavana alipata wasaa wa kutembelea na kujionea bidhaa mbalimbali katika Banda la Maonesho ya Bidhaa na Huduma alipotembelea Makao Makuu ya shirika hilo Mlalakuwa Dar es salaam.

Taarifa zaidi kuhusu ugeni huo imewekwa katika chaneli ya YouTube ya SUMAJKT hapa chini;

Similar Posts

  • Brigedia Jenerali Petro Ngata apokelewa kwa Furaha SUMAJKT

    Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la kujenga Taifa Brigedia Jenerali Petro Ngata, amepokelewa kwa furaha na Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT katika ukumbi wa Mikutano, Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. Brigedia Jenerali Ngata akipokelewa kwa mara ya kwanza tangu apandishwe cheo hicho kutoka cheo cha Kanali, alianza kukaribishwa kwa gwaride la heshima na baadae kupokelewa na kamati ya Utendaji ya SUMAJKT. Akizungumza katika ukumbi wa mikutano Brigedia Jenerali Ngata ametoa shukrani za dhati kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu Meja Jenerali Rajab Mabele…

  • WATANZANIA WANUFAIKA NA FURSA ZINAZOTOLEWA NA SUMAJKT

    Tarehe 16 Januari 2023, Mkuu wa tawi la utawala JKT, Brigedia Jenerali Hassan Mabena alizindua magari 17 kwa ajili ya kuimarisha a utendaji wenye tija na kuboresha huduma za ulinzi. Aidha aliendelea kusema kwamba SUMAJKT itaendelea kutengeneza fursa mbalimbali kupitia kampuni ya SUMAJKT na hivyo kunufaisha Watanzania kwa ujumla. Bregedia Jenerali Hassan Mabena liendelea kuwashukuru na kuwaasa taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kuendelea kufanyakazi kwa kupitia kampuni tanzu za SUMAJKT.

  • Mkuu wa Jeshi Namibia avutiwa na shughuli za SUMAJKT

    Mkuu wa Jeshi Namibia avutiwa na shughuli za SUMAJKT. Mkuu wa Jeshi la Nchi kavu Nchini Namibia Meja jenerali Aktofel Nambahu Amevutiwa na Shughuli za Uzalishaji mali zinazofanya na Jeshi la Kujenga Taifa Kupitia Shirika lake SUMAJKT. Meja Jenerali Nambahu amepokelewa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Shija Lupi kwa Niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele leo tarehe 20 Agosti 2025 Makao Makuu ya Shirika Mlalakuwa Jijini Dar es salaam. Mkuu wa Jeshi Namibia avutiwa na shughuli za SUMAJKT. Ziara yangu JKT ni mualiko wa Mkuu…

  • |

    Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi

    Naibu Waziri Mambo ya Ndani Mhe. Daniel Sillo ayashauri mashirika ya Kijeshi ndani ya Nchi wanachama katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutumia Sayansi na Teknolojia katika uzalizalishaji wa bidhaa zao. Mhe. Sillo amesema hayo leo tarehe 25 Februari 2025 alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Mashirika yanayo milikiwa na  Majeshi ya  nchi za  Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika hoteli ya Geraffe iliyopo jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi, Amefafanua kuwa Mkutano huo hufanyika kila mwaka ili kutathmini utendaji kazi wa Mashirika na Viwanda vilivyopo ndani ya Majeshi yaliyopo katika Jumuiya ya…

  • |

    Maafisa UPDF watembelea SUMAJKT Makao Makuu

    Maafisa UPDF watembelea SUMAJKT Makao Makuu. Maafisa Jenerali, Maafisa wakuu na Askari kutoka Jeshi la Uganda (UPDF) wakiongozwa na Meja Jenerali Willium Nabasa, leo tarehe 29 Aprili 2025 wametembelea Makao Makuu ya SUMAJKT Mlalakuwa Dar es Salaam ili kujifunza shughuli za Jeshi la Kujenga Taifa na SUMAJKT kwa manufaa ya kuliendeleza Jeshi la Uganda. Maafisa hao wamepokelewa na Mkuu wa Shule ya Jitegemee Kanali Emmanuel Mwaigobeko, kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele. Akizungumzia ugeni huo Kanali Mwaigobeko, amesema lengo la ziara hiyo ni kujifunza Shughuli zinazofanywa na JKT pamoja na SUMAJKT. Jeshi la…

  • Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta

    Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amesema shirika lina dhamira ya kuendelea kujitanua na kuimarisha miundombinu ya kimkakati ya biashara ikiwemo sekta ya nishati. Brigedia Jenerali Petro Ngata, amesema hayo katika uzinduzi wa gari la kusafirishia mafuta la Kampuni ya SUMAJKT Logistiki leo tarehe 26 Mei 2025, Makao Makuu ya Shirika Mlalakuwa Dar es salaam. Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata, amefafanua gari hilo litaongeza ufanisi katika usambazaji wa nishati ya…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *