Waziri wa Mji, Juma Aweso, alipotembelea kijiji cha Msomera, wilayani Handeni ambapo nyumba jumla 5000 pamoja na miundombinu ya maji imejengwa kupitia shirika la SUMAJKT.
Zaidi tazama video hii hapa kufahamu undani wa taarifa hio.
Waziri wa Mji, Juma Aweso, alipotembelea kijiji cha Msomera, wilayani Handeni ambapo nyumba jumla 5000 pamoja na miundombinu ya maji imejengwa kupitia shirika la SUMAJKT.
Zaidi tazama video hii hapa kufahamu undani wa taarifa hio.
Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amesema shirika lina dhamira ya kuendelea kujitanua na kuimarisha miundombinu ya kimkakati ya biashara ikiwemo sekta ya nishati. Brigedia Jenerali Petro Ngata, amesema hayo katika uzinduzi wa gari la kusafirishia mafuta la Kampuni ya SUMAJKT Logistiki leo tarehe 26 Mei 2025, Makao Makuu ya Shirika Mlalakuwa Dar es salaam. Mkurugenzi Mtendaji SUMAJKT azindua gari la kusafirisha mafuta. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata, amefafanua gari hilo litaongeza ufanisi katika usambazaji wa nishati ya…
Meja Jenerali (Mstaafu) Zawadi Madawili ametoa wito kwa Maafisa wanawake wa Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania kufanya kazi kwa bidii ili kujiimarisha kiutendaji katika nafasi zao mbalimbali wanazohudumu. Meja Jenerali Mstaafu Madawili ameyasema hayo tarehe 02 Mei 2025 katika kikao cha Umoja wa Maafisa wa kike wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wanaofanyia kazi Jeshi la Kujenga (JKT) pamoja na Kamandi nyingine ambacho kimefanyika katika Hoteli ya Ndege Beach Mbweni JKT Jijini Dar es salaam. Aidha ameeleza siri ya kudumu muda mrefu katika Utumishi ni kufuata Misingi iliyowekwa ambayo ni pamoja na Nidhamu katika kazi, roho…
Maafsa JKT wameaswa kutekeleza kwa weledi jukumu la malezi ya vijana. Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala JKT Kanali Juma Mrai amewaasa Maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wanaofanyia kazi Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), kutekeleza kwa weledi jukumu la Malezi ya Vijana. Kanali Mrai ametoa rai hiyo tarehe 21 Machi 2025 wakati akihitimisha Semina Elekezi ya Maafisa wa JWTZ waliopewa Uhamisho kwenda JKT, iliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Taifa (CUJKT) kilichopo Kimbiji Jijini Dar es Salaam Jeshi la Kujenga Taifa limekuwa likiendesha Semina Elekezi kwa watendaji wake ili kuwajengea uwezo wa…
Mwenyekiti kamati ya NaneNane akaribisha wananchi Dodoma. Mwenyekiti wa Kamati ya Maonesho ya Wakulima Nanenane Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Shija Lupi amewakaribisha wananchi wote hapa nchini kutembelea Maonesho ya Wakulima Nanenane Kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni Dodoma na Kikanda katika Kanda zote ambazo Jeshi hilo linashiriki.
DC Ikungi avutiwa na maonesho ya JKT Nane Nane. Mkuu wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida Mhe.Thomas Cornel amevutiwa na Bidhaa na Huduma za Jeshi la Kujenga Taifa katika maonesho ya Wakulima Nanenane yanayofanyika kitaifa katika Viwanja vya Nzuguni Dodoma. Akizungumza baada ya kutembelea Banda la JKT leo tarehe 6 Agost 2025, Mhe. Cornel amepongeza JKT kwa uzalishaji wa mazao mbalimbali yanayosaidia upatikanaji wa chakula cha asili kinachokidhi viwango vya soko la kimataifa. DC Ikungi avutiwa na maonesho ya JKT Nane Nane. Vilevile, Mhe. Cornel amepongeza JKT na Shirika lake SUMAJKT kwa Ubunifu wa bidhaa mbalimbali na Utekelezaji mzuri wa…
SUMAJKT Cleaning and Fumigation yajiimarisha kisasa kwenye usafi. Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa (SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co.Ltd) imezidi kujiimarisha kwa kununua mashine za kisasa za kufagia barabara ili kuendelea kutoa huduma bora kwa Taasisi na Kampuni mbalimbali nchini. Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, leo tarehe 30 Aprili 2025 baada ya kuzindua Mashine za kisasa za kufagia barabara amewahimiza watendaji wa kampuni hiyo kutunza mashine hizo ili ziweze kuleta tija kwa shirika. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata, amefafanua uwepo wa Mashine hizo kutaiongezea kampuni hiyo uwezo zaidi…