MKUU WA JKT AMSHUKURU RAIS NA AMIRI JESHI MKUU MAFUNZO YA JKT

Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleza mafunzo ya vijana wa JKT. Mkuu wa JKT amshukuru Rais na Amiri Jeshi Mkuu mafunzo ya JKT.

Meja Jenerali Mabele, ameyasema hayo leo tarehe 17 Aprili 2025 alipokuwa anahitimisha mafunzo ya Awali ya kijeshi kwa vijana wa Operesheni miaka 60 ya Muungano katika kikosi Cha Ruvu JKT kilichopo mlandizi mkoani Pwani.

Amesema Malezi ni suala Mtambuka, yanaanzia ngazi ya familia, Vijana wanapofika makambini. Jeshi la Kujenga Taifa linawafundisha Vijana kuipenda na kuitumikia nchi yao ya Tanzania, linawajengea Uzalendo, Kuwafunza nidhamu, Ukakamavu na Umoja wa Kitaifa ili kijana anapotoka JKT awe Mtiifu, Hodari na Mwaminifu.

Aidha, Meja Jenerali Mabele, amewaasa vijana hao kuzingatia na kutunza Afya zao kwa kipindi chote cha miezi 20 kilichobaki kwani afya ndio msingi na mtaji mkubwa kwa kijana ili awe na sifa za kuchukuliwa na vyombo vya Ulinzi na usalama.

Naye Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda, Brigedia Jenerali Abubakar Charo, amewataka kwenda kuzingatia Mafunzo ya Stadi za Kazi na Stadi za Maisha kwani ndiyo yatakayowasaidia kujitegemea baada ya kumaliza mkataba wa Jeshi la Kujenga Taifa.

Kamanda Kikosi Ruvu JKT Kanali Peter Mnyani akitoa taarifa fupi ya mafunzo amesema mafunzo hayo yalianza tarehe 30 Desemba 2024 na kuhitimishwa tarehe tarehe 17 Aprili 2025.

Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube

Similar Posts

  • Waziri wa Ulinzi Angola apongeza malezi ya JKT kwa vijana

    Waziri wa Ulinzi wa Angola apongeza namna Jeshi la Kujenga Taifa linavyowalea Vijana wa Kitanzania. Waziri wa Ulinzi wa Angola Mhe.Joao Ernesto Das Santos ametoa pongezi hizo katika mwendelezo wa ziara yake hapa nchini, ambapo ametembelea Kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mkoa wa Pwani tarehe 9 Januari 2025.

  • RUVU JKT WAACHANA NA MATUMIZI YA KUNI NA MKAA

    Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax ameupongeza uongozi wa kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mkoani Pwani kwa kuachana na matumizi ya nishati ya kuni na mkaa na kuanza kutumia nishati ya gesi kwa asilimia 100. Ruvu JKT waachana na matumizi ya kuni na mkaa. Mhe.Dkt. Tax ametoa pongezi hizo tarehe 3 Aprili 2025 wakati alipofanya ziara kikosini hapo na kujionea namna kikosi hicho chini ya Uongozi wa kamanda kikosi Kanali Peter Mnyani unavyotekeleza kwa vitendo maelekezo ya serikali ya kuachana na matumizi ya kuni na mkaa kwa Taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100. Amepongeza ubunifu wa…

  • Waziri wa Ulinzi Zimbabwe atembelea SUMAJKT

    Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Oppah Kashiri, amefanya ziara Makao Makuu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Mlalakuwa Dar es salaam. Katika Ziara hiyo Mhe. Waziri Kashiri, akiwa na Waziri wa Ulinzi na JKT wa Tanzania Dkt. Stergomena Tax, alipatiwa taarifa ya shirika na kutembelea kiwanda cha Taa cha SUMAJKT Skyzone Co Ltd. Kilichopo Mlalakuwa na kiwamda cha Maji ya Kunywa cha SUMAJKT Bottling Co Ltd. Kilichopo Mgulani JKT.

  • DED SUMAJKT atembelea Mafinga.

    DED SUMAJKT atembelea Mafinga. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Shija Sahani Lupi ametembelea Miradi mbalimbali inayoendeshwa na Shirika hilo katika Halimashauri ya mji mdogo Mafinga Mkoani Iringa. Tukio hilo limejiri tarehe 17 Oktoba 2025 mara baada ya kushiriki Mahafali ya 29 ya kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Kawawa JKT akiwa Mgeni rasmi. Brigedia Jenerali Lupi ametembelea Majengo ya madarasa mapya yatakayotumika kujifunza kwa njia ya mtandao (E-learning), shule ya Awali na Msingi, eneo la shamba jipya la mifugo (Ng’ombe) na baada ya kutembelea maeneo hayo alipata fursa ya kuongea…

  • SUMAJKT LAJIWEKEA MALENGO MWAKA WA FEDHA 2024/’25

    Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) limeweka malengo ya kufikika na linaendelea kusimamia miradi kwa ufanisi ili kuleta tija kwa shirika. Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya (SUMAJKT) Meja Jenerali (mstaafu) Farah Mohamed, amesema hayo tarehe 19 Oktoba 2024 katika kikao cha kwanza cha malengo ya shirika cha mwaka wa fedha ujao wa 2024/2025 kilichofanyika katika ukumbi wa SUMAJKT Tower uliopo jijini Dodoma. Kikao hicho kilihudhuriwa wajumbe wa Bodi akiwemo Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata pamoja na wajumbe waalikwa…

  • | | |

    WANANCHI WA COMORO WAFURAHISHWA NA BIDHAA KUTOKA SUMAJKT

    Tarehe 12 hadi 19 mwezi Disemba 2022 kulifanyika Maonyesho ya Kibiashara eneo la ETG Moroni ambapo maonyesho hayo yaliratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro. Katika maonyesho hayo SUMAJKT ilialikwa kwa ujumbe rasmi wa balozi na uwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Ahmed. Maonyesho hayo yalikuwa na lengo la kukuza uhusiano wa kiuchumi baina ya serikali na wananchi wa nchi hizo mbili (Tanzania na Comoro) ambapo wananchi Comoro wafurahishwa na bidhaa kutoka SUMAJKT. Wananchi wa Moroni walipata fursa ya kujionea bidhaa mbalimbali zinazozakishwa na SUMAJKT na wengi walionyesha kuridhishwa na viwango vya bidhaa hizo. Katika picha unaweza kushuhudia…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *