Similar Posts
Kusitishwa kwa mafunzo ya JKT kulileta athari kubwa ikiwemo ya mmomonyoko wa maadili
” KUSITISHWA KWA MAFUNZO YA JKT KULILETA ATHARI KUBWA IKIWEMO YA MMOMONYOKO WA MAADILI”Wakuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (Wastaafu)Meja Jenerali Martin Madata (Mstaafu) na Meja Jenerali Samwel Kitundu (Mstaafu), wakielezea umuhimu wa Mafunzo ya JKT, athari zilizopatikana baada ya kusitishwa kwa Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria na Kujitolea pamoja na Mafanikio yaliyopatikana Baada ya kurejeshwa kwa Mafunzo hayo. Wameyasema hayo wakati wa Mahojiano Maalumu ya Mafanikio yaliyopatikana ndani ya JKT kwa kipindi cha Miaka 60 ya Uwepo wake nchini.https://www.instagram.com/reel/DGvnVdetkhE/?igsh=ZmJua2s1NWlvcndw Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube
Buriani Meja Jenerali Charles Mbuge (Mstaafu)
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Maafisa, Askari, Vijana na watumishi wote wa Umma JKT, wanaungana na familia kuomboleza kifo cha aliyewahi kuwa Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT 2019-2021 Meja Jenerali Charles Mbuge (Mstaafu). Apumzike kwa Amani.
Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT amuaga Jenerali Musuguri
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, akitoa heshima za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu Jenerali David Musuguri (Mstaafu) katika hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo Dar es salaam. Tukio la Kuaga Mwili wa Marehemu Jenerali David Musuguri (Mstaafu) aliyefariki Oktoba 29, 2024 limeongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango. Viongozi wengine waliohudhuria Tukio hilo ni Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, Waziri wa Ulinzi Dkt. Stergomena Tax, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda, Maafisa Majenerali, Maafisa…
JKT limesema litawachukulia hatua za kisheria watu waliobainika na watakaobainika kughushi vyeti
Jeshi la Kujenga Taifa JKT limesema litawachukulia hatua za kisheria watu waliobainika na watakaobainika kughushi vyeti vya kuhitimu mafunzo. JKT imefikia uamuzi huo baada ya kubaini uwepo wa vyeti vya kughushi vilivyotumiwa na baadhi ya vijana ambao siyo waaminifu ili kujipatia ajira katika taasisi nakampuni zinazohitaji watendaji waliopitia mafunzo ya jeshi hilo. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma, Kaimu Mkuu wa Tawi la Utawala, Kanali Juma Mrai amesema Jeshi la Kujenga Taifa lipo tayari kutoa ushirikiano kwa taasisi na kampuni zote zinazohitaji uhakiki wa vyeti kwa watumishi wao waliopitia mafunzo ya JKT. JKT limesema litawachukulia hatua za kisheria watu…
MAAFISA FANYENI KAZI KWA BIDII, MJIIMARISHE KIUTENDAJI – MEJA JENERALI ( MSTAAFU) MADAWILI
Meja Jenerali (Mstaafu) Zawadi Madawili ametoa wito kwa Maafisa wanawake wa Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania kufanya kazi kwa bidii ili kujiimarisha kiutendaji katika nafasi zao mbalimbali wanazohudumu. Meja Jenerali Mstaafu Madawili ameyasema hayo tarehe 02 Mei 2025 katika kikao cha Umoja wa Maafisa wa kike wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania wanaofanyia kazi Jeshi la Kujenga (JKT) pamoja na Kamandi nyingine ambacho kimefanyika katika Hoteli ya Ndege Beach Mbweni JKT Jijini Dar es salaam. Aidha ameeleza siri ya kudumu muda mrefu katika Utumishi ni kufuata Misingi iliyowekwa ambayo ni pamoja na Nidhamu katika kazi, roho…
Marehemu Meja Jenerali Busungu azikwa Luchelele Mwanza
Waziri Wa Ulinzi na Jeshi La Kujenga Taifa Mhe. Stargomena Lawrence Tax, ameongoza Maafisa, Askari, Vijana, Watumishi wa Umma na Waombolezaji katika Mazishi ya Mwili Wa Marehemu Meja Jenerali Martin Busungu (Mstaafu) yaliyofanyika katika Kijiji Cha Luchelele Jijini Mwanza tarehe 28 Desemba 2024. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda, katika Mazishi hayo Mkuu wa Jeshi La Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, amesema Marehemu Meja Jenerali Busungu (Mstaafu) enzi za uhai wake akiwa mtumishi ndani ya Jeshi la ulinzi la Wananchi wa Tanzania ametumikia Jeshi kwa kipindi…


