Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Maafisa, Askari, Vijana na watumishi wote wa Umma JKT, wanaungana na familia kuomboleza kifo cha aliyewahi kuwa Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT 2019-2021 Meja Jenerali Charles Mbuge (Mstaafu). Apumzike kwa Amani.
Similar Posts
Kusitishwa kwa mafunzo ya JKT kulileta athari kubwa ikiwemo ya mmomonyoko wa maadili
” KUSITISHWA KWA MAFUNZO YA JKT KULILETA ATHARI KUBWA IKIWEMO YA MMOMONYOKO WA MAADILI”Wakuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (Wastaafu)Meja Jenerali Martin Madata (Mstaafu) na Meja Jenerali Samwel Kitundu (Mstaafu), wakielezea umuhimu wa Mafunzo ya JKT, athari zilizopatikana baada ya kusitishwa kwa Mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria na Kujitolea pamoja na Mafanikio yaliyopatikana Baada ya kurejeshwa kwa Mafunzo hayo. Wameyasema hayo wakati wa Mahojiano Maalumu ya Mafanikio yaliyopatikana ndani ya JKT kwa kipindi cha Miaka 60 ya Uwepo wake nchini.https://www.instagram.com/reel/DGvnVdetkhE/?igsh=ZmJua2s1NWlvcndw Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube
SUMAJKT MARATHON YAZINDULIWA
Usajili wa SUMAJKT MARATHON, Sunday 7 June 2026 UMEFUNGULIWA RASMI na CEO wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa kushirikiana na CRDB Bank.JISAJILI KUPITIA TOVUTI YA www.sumajktmarathon.co.tz Twendezetu Pace ya Kwata Mapigano Na Mwendo
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa aongoza waombolezaji kumuaga Meja Jenerali Charles Mbuge
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt Stergomena Lawrence Tax (Mb) tarehe 16 Octoba, 2024 katika Hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo, jijini Dar es Salaam ameongoza Maafisa, Askari, Watumishi wa Umma pamoja na waomboleazaji, kutoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa Marehemu Meja Jenerali Mstaafu Charles Mbuge, aliyefariki Dunia tarehe 12 Octoba 2024. Miongoni mwa viongozi walioungana na Waziri wa Ulinzi na JKT kumuaga na kutoa heshima za mwisho kwa marehemu Jenerali Mbuge, ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Bw. Albert Chalamila, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda, Mnadhimu…
Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT amuaga Jenerali Musuguri
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, akitoa heshima za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu Jenerali David Musuguri (Mstaafu) katika hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo Dar es salaam. Tukio la Kuaga Mwili wa Marehemu Jenerali David Musuguri (Mstaafu) aliyefariki Oktoba 29, 2024 limeongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango. Viongozi wengine waliohudhuria Tukio hilo ni Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, Waziri wa Ulinzi Dkt. Stergomena Tax, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda, Maafisa Majenerali, Maafisa…
CDF MKUNDA AKABIDHIWA VIFAA VYA KUKIMBILIA
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Jacob Mkunda, akikabidhiwa vifaa vya kukimbilia (Running Kit) na Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa ambaye pia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kwa ajili ya Kushiriki SUMAJKT Marathon itakayofanyika Tarehe 07 Juni 2026 (Jumapili hii) katika eneo la SUMAJKT House lililopo Medeli East jirani na Taa za Barabarani zilizopo njia panda ya kuelekea kwa Waziri Mkuu Jijini Dodoma. Kupata ratiba nzima ya Marathon gusa link hii hapa


