CDF aipongeza SUMAJKT kwa kuanzisha kampuni mpya.

CDF aipongeza SUMAJKT kwa kuanzisha kampuni mpya. Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Jacob John Mkunda, amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa maono ya kuanzisha Kampuni ya Bima ya Maisha (SUMAJKT Life Insurance Co. Ltd) itakayokuwa Msaada mkubwa kwa Watanzania kwa Vizazi vya sasa na Vijavyo.

Jenerali Mkunda, ameyasema hayo Tarehe 10 Mei 2025 katika Sherehe ya Uzinduzi wa Kampuni ya Bima ya Maisha ya SUMAJKT tukio lililofanyika Ukunbi wa (The Super Dome Masaki Jijini Dar es salaam. CDF aipongeza SUMAJKT kwa kuanzisha kampuni mpya.

Amesema imani yake ni kuona watanzania wakipatiwa huduma hiyo ya Bima kwani Jeshi la Kujenga taifa kupitia Shirika lake SUMAJKT limekua likitoa huduma stahiki kwa wateja kupitia, Kampuni zake tanzu, Viwanda, pamoja na Miradi ya kibiashara.

Aidha Jenerali Mkunda ametoa wito kwa watanzania kuitumia kampuni ya Bima ili waweze kupata suluhisho la changamoto zao za kibima. CDF aipongeza SUMAJKT kwa kuanzisha kampuni mpya.

Naye Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele, amesema Kampuni ya Bima ya SUMAJKT tayari imesajiliwa, huku akiahidi utolewaji wa huduma bora za viwango stahiki.

Sherehe hiyo ilihudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya SUMAJKT, Meja Jenerali Farah Mohamed (Mstaafu), Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama, Wakuu wa Kamandi, Wakuu wa Matawi Makao Makuu ya Jeshi na Makao Makuu ya JKT, Wakuu wa Vyuo na Shule, Maafisa Jenerali, Kamishna wa Bima Tanzania Dkt. Baghayo Saqware, Wakuu wa Taasisi mbalimbali za Serikali na Binafsi, Mwenyekiti wa Umoja wa Kampuni za Bima Tanzania (ATI) Bi. Flora Minja, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Kampuni ya Bima ya SUMAJKT Meja Godson Mhando, Maafisa wakuu, Maafisa Wadogo, Askari, Wageni waalikwa na Waandishi wa Habari.

Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube.

Similar Posts

  • Wakufunzi CUJKT watembelea SUMAJKT

    Wakufunzi CUJKT watembelea SUMAJKT. Wakufunzi na Maafisa wanaoshiriki Kozi Elekezi kutoka Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Taifa (CUJKT) tarehe 18 Machi 2025 wamefanya Ziara ya kimasomo katika Shirika la Uzalishaji la Jeshi la kujenga Taifa (SUMAJKT) kwa lengo la kuona Shughuli zinazofanywa na Kampuni zake Tanzu zilizopo eneo la Makao Makuu ya Shirika hilo Mlalakuwa na zilizopo Mwenge jijini Dar es Salaam. Ziara hiyo iliyolenga kujifunza kuhusu shughuli zinazofanywa na SUMAJKT, namna ambavyo huratibiwa na kutekelezwa pamoja na mchango wa Shirika kwa JKT na taifa kwa Ujumla, itaendelea hapo kesho tarehe 19 machi 2025 ambapo Wakufunzi na wanafunzi…

  • Waziri wa Ulinzi Zimbabwe atembelea SUMAJKT

    Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Oppah Kashiri, amefanya ziara Makao Makuu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Mlalakuwa Dar es salaam. Katika Ziara hiyo Mhe. Waziri Kashiri, akiwa na Waziri wa Ulinzi na JKT wa Tanzania Dkt. Stergomena Tax, alipatiwa taarifa ya shirika na kutembelea kiwanda cha Taa cha SUMAJKT Skyzone Co Ltd. Kilichopo Mlalakuwa na kiwamda cha Maji ya Kunywa cha SUMAJKT Bottling Co Ltd. Kilichopo Mgulani JKT.

  • Mkurugenzi Temeke afanya usafi na wahitimu wa Jitegemee JKT

    Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Wilaya ya Temeke Mhe. Jomary Satura, ameongoza wahitimu waliowahi kupata elimu yao katika shule ya SekondariJitegemee JKT, pamoja na wanachiwote kwenye zoezi la kufanya usafi katika soko la Temeke Sterio tarehe 2 Octoba 2024 ikiwa ni sehemu ya Maadhimisho ya miaka 50 tangu kuanzishwa kwa shule hio. Taarifa zaidi gusa video hii hapa chini..

  • DED SUMAJKT atembelea Mafinga.

    DED SUMAJKT atembelea Mafinga. Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali Jeshi la Kujenga Taifa Brigedia Jenerali Shija Sahani Lupi ametembelea Miradi mbalimbali inayoendeshwa na Shirika hilo katika Halimashauri ya mji mdogo Mafinga Mkoani Iringa. Tukio hilo limejiri tarehe 17 Oktoba 2025 mara baada ya kushiriki Mahafali ya 29 ya kidato cha Nne katika shule ya Sekondari Kawawa JKT akiwa Mgeni rasmi. Brigedia Jenerali Lupi ametembelea Majengo ya madarasa mapya yatakayotumika kujifunza kwa njia ya mtandao (E-learning), shule ya Awali na Msingi, eneo la shamba jipya la mifugo (Ng’ombe) na baada ya kutembelea maeneo hayo alipata fursa ya kuongea…

  • SUMAJKT Yatwaa tuzo Sabasaba

    SUMAJKT Yatwaa tuzo Sabasaba. Jeshi la Kujenga Taifa kupitia Shirika lake la Uzalishaji Mali (SUMAJKT) limeibuka mshindi wa Kwanza katika Samani na Ubunifu wa ndani katika Maonyesho ya 49 ya Biashara Kimataifa (Sabasaba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julias Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dara es Salaam. Tuzo ya Ushindi huo imekabidhiwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Tanzania Mhe. Selemani Jafo, kwa Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, katika ufunguzi wa Maonesho hayo leo tarehe 7 Julai 2025 katika Viwanja vya Sababa jijini Dar es Salaam. Akizungumzia Ushindi huo Mkuu wa JKT…

  • Brigedia Jenerali Petro Ngata apokelewa kwa Furaha SUMAJKT

    Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la kujenga Taifa Brigedia Jenerali Petro Ngata, amepokelewa kwa furaha na Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT katika ukumbi wa Mikutano, Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. Brigedia Jenerali Ngata akipokelewa kwa mara ya kwanza tangu apandishwe cheo hicho kutoka cheo cha Kanali, alianza kukaribishwa kwa gwaride la heshima na baadae kupokelewa na kamati ya Utendaji ya SUMAJKT. Akizungumza katika ukumbi wa mikutano Brigedia Jenerali Ngata ametoa shukrani za dhati kwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob Mkunda, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu Meja Jenerali Rajab Mabele…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *