Kampuni ya usafi SUMAJKT yasaini mkataba na Halmashauri ya Jiji Dar

Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa ya SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co. Ltd  imetia Saini Mkataba wa kufanya Usafi katika Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam Katika Maeneo ya Soko la Buguruni Pamoja na Soko la Ilala leo tarehe18 Februari 2025.

Hafla hiyo ambayo  imehudhuriwa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mhe. Elihuruma Mabelya, Mstahiki Meya wa Jiji Mhe. Omary Kumbilamoto, Madiwani, na wadau wa Maendeleo imehusisha pia Uzinduzi wa Magari yaliyo nunuliwa na jiji yatakayotumika Katika Usafi.

Akizungumza mara baada ya Kutia Saini Mkataba huo Mkuu wa Wilaya ya Ilala Mhe. Edward Jonas Mpogolo, amesema Serikali ina Imani na Kampuni ya Usafi ya SUMAJKT kwani imekua ikitekeleza Miradi kwa Ufanisi na kwa wakati.

Aidha Mstahiki Meya wa Jiji hilo Mhe. Omary Kumbilamoto, ameeleza kwamba siri ya Kusaini Mkataba huo na SUMAJKT ni utendaji wao wa kazi.

Nae Mkurugenzi Mwendeshaji wa  Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa ya SUMAJKT Cleaning and  Fumigation Co. Ltd. Kapteni Rosemary Katani,  ameeleza kuwa  Kampuni hiyo imejipanga Kufanya mapinduzi makubwa katika Usafi.

Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube

Similar Posts

  • Kampuni ya Umeme ya SUMAJKT Electrical Co Ltd kuongezewa kandarasi za kusambaza umeme.

    Kampuni ya Umeme ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa SUMAJKT Electrical Co Ltd. Imepongezwa kwa kutekeleza kwa wakati na weledi Mkubwa kandarasi ambazo imekua ikiingia mikataba. Akizungumza Naibu waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Nishati Mhe.Doto Biteko katika hafla ya kutia saini mkataba wa kufunga mifumo ya nishati safi ya kupikia katika makambi 22 ya JKT kwa mikoa 14 uliyosainiwa baina ya JKT na Wakala wa Nishati vijijini REA,Tukio lililofanyika Jijini Dodoma. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko amelipongeza Shirika la Uzalishaji Mali la JKT(SUMA JKT) kupitia SUMAJKT Electric Co.Ltd kwa…

  • SUMAJKT Kutafuta Fursa za Biashara visiwani Comoro

    Ujumbe wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMA JKT) unazuru nchini Comoro kwa minajili ya utafutaji wa fursa za ushirikiano wa kibiashara ikiwa ni siku chache baada ya kumalizika kwa Mkutano wa Wenyeviti na Watendaji Wakuu ambao ulihimiza Mashirika ya Umma kuangazia fursa nje ya nchi. Ziara hiyo inafuatia mwaliko wa Gavana wa Kisiwa cha Ngazidja Mheshimiwa Ibrahim Mze na inataratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Comoro inaongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa SUMA JKT, Brigedia Jenerali Petro Ngata. Mara baada ya kuwasili, Ujumbe wa SUMA JKT ulipata fursa ya kufanya mazungumzo na Gavana wa Kisiwa cha…

  • |

    Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi

    Naibu Waziri Mambo ya Ndani Mhe. Daniel Sillo ayashauri mashirika ya Kijeshi ndani ya Nchi wanachama katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutumia Sayansi na Teknolojia katika uzalizalishaji wa bidhaa zao. Mhe. Sillo amesema hayo leo tarehe 25 Februari 2025 alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Mashirika yanayo milikiwa na  Majeshi ya  nchi za  Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika hoteli ya Geraffe iliyopo jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi, Amefafanua kuwa Mkutano huo hufanyika kila mwaka ili kutathmini utendaji kazi wa Mashirika na Viwanda vilivyopo ndani ya Majeshi yaliyopo katika Jumuiya ya…

  • MKUU WA JKT AISHUKURU SERIKALI KULIWEZESHA JKT KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE

    Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Mabele ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuliwezesha Jeshi la Kujenga Taifa kutekeleza majukumu yake Meja Jenerali Mabele ametoa shukrani hizo tarehe 16 Januari 2025 Makao Makuu ya JKT wakati wa hafla ya uzinduzi wa Magari aina ya Isuzu D Max Pick Up idadi tisa (9) kwaajili ya Matumizi ya shughuli za kiutawala ndani ya Jeshi la Kujenga Taifa. Magari hayo yamekabidhiwa kwa baadhi ya Wakurugenzi wa Makao Makuu ya JKT na Makamanda Vikosi vya Jeshi la Kujenga Taifa.

  • CDF aipongeza SUMAJKT kwa kuanzisha kampuni mpya.

    CDF aipongeza SUMAJKT kwa kuanzisha kampuni mpya. Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Jenerali Jacob John Mkunda, amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa maono ya kuanzisha Kampuni ya Bima ya Maisha (SUMAJKT Life Insurance Co. Ltd) itakayokuwa Msaada mkubwa kwa Watanzania kwa Vizazi vya sasa na Vijavyo. Jenerali Mkunda, ameyasema hayo Tarehe 10 Mei 2025 katika Sherehe ya Uzinduzi wa Kampuni ya Bima ya Maisha ya SUMAJKT tukio lililofanyika Ukunbi wa (The Super Dome Masaki Jijini Dar es salaam. CDF aipongeza SUMAJKT kwa kuanzisha kampuni mpya. Amesema imani yake ni kuona watanzania wakipatiwa huduma hiyo ya Bima kwani Jeshi…

  • Wakufunzi CUJKT watembelea SUMAJKT

    Wakufunzi CUJKT watembelea SUMAJKT. Wakufunzi na Maafisa wanaoshiriki Kozi Elekezi kutoka Chuo cha Uongozi cha Jeshi la Kujenga Taifa (CUJKT) tarehe 18 Machi 2025 wamefanya Ziara ya kimasomo katika Shirika la Uzalishaji la Jeshi la kujenga Taifa (SUMAJKT) kwa lengo la kuona Shughuli zinazofanywa na Kampuni zake Tanzu zilizopo eneo la Makao Makuu ya Shirika hilo Mlalakuwa na zilizopo Mwenge jijini Dar es Salaam. Ziara hiyo iliyolenga kujifunza kuhusu shughuli zinazofanywa na SUMAJKT, namna ambavyo huratibiwa na kutekelezwa pamoja na mchango wa Shirika kwa JKT na taifa kwa Ujumla, itaendelea hapo kesho tarehe 19 machi 2025 ambapo Wakufunzi na wanafunzi…

2 Comments

  1. Habari mkuu naitwa jenifa Ezekiel ni raia wa Tanzania Niko dar es salaam chanika. Naomba nafasi ya KAZI za usafi naimani tafanya KAZI Kwa juhudi zote Takuwa mfanyakazi Bora mwenye nidham na maadili mema natumaini Omni langu tajibuwa asane

    1. Habari Jenifa, unaweza kufika ofisi za SUMAJKT Cleaning and Fumigation zilizopo Mwenge Jijini Dar es Salaam kuulizia kuhusu nafasi za kazi kama ulivyozitaja.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *