Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kuhitimisha Ufungaji wa Mafunzo ya Vijana wa Kujitolea OP Miaka 60 ya Muungano Ruvu JKT

Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kuhitimisha Ufungaji wa Mafunzo ya Vijana wa Kujitolea OP Miaka 60 ya Muungano Ruvu JKT. Mkuu wa Tawi la Mafunzo Jeshi la Kujenga Taifa Kanali Longinus Nyingo tarehe 16 Aprili 2025 amekagua Maandalizi ya Mwisho kuelekea kuhitimishwa kwa zoezi la Ufungaji wa Mafunzo ya awali ya Kijeshi kwa Vijana wa Kujitolea Operesheni Miaka 60 ya Muungano katika Kikosi cha Ruvu JKT Mlandizi mkoani Pwani.

Kanali Nyingo amesema kuwa, zoezi la ufungaji wa Mafunzo katika Vikosi vyote vya JKT lilianza tarehe 8 Aprili 2025 ambapo Mkuu wa JKT alikuwa akiwakilishwa na Wakuu wa Matawi na Wakurugenzi kutoka Makao Makuu ya JKT, kesho tarehe 17 Aprili 2025 zoezi hilo litahitimishwa na Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kikosi hapo. Mkuu wa JKT Meja Jenerali Rajabu Mabele kuhitimisha Ufungaji wa Mafunzo ya Vijana wa Kujitolea OP Miaka 60 ya Muungano Ruvu JKT.

Nae Kamanda Kikosi Ruvu JKT Kanali Peter Mnyani Amewakaribisha wananchi wa Mkoa wa Pwani na Maeneo jirani kwenda kushuhudia Vijana wao wakihitimisha Mafunzo yao.

Katika kukuza utalii wa ndani, Kanali Mnyani ametumia wasaa huo kuwakaribisha wananchi kutembelea bustani ya Wanyama pori walio wapole ya RUVUJKT WILDLIFE.

Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube
https://www.instagram.com/p/DIHNoSIIeOh/?igsh=MWlvM29jeGUwMWNvMQ==


chanzo: https://www.instagram.com/reel/DIgxcR1oD_b/?igsh=OGtjcHVnN2V4Nm1z

Similar Posts

  • SUMAJKT Cleaning and Fumigation yajiimarisha kisasa kwenye usafi

    SUMAJKT Cleaning and Fumigation yajiimarisha kisasa kwenye usafi. Kampuni ya Usafi na Unyunyiziaji Dawa (SUMAJKT Cleaning and Fumigation Co.Ltd) imezidi kujiimarisha kwa kununua mashine za kisasa za kufagia barabara ili kuendelea kutoa huduma bora kwa Taasisi na Kampuni mbalimbali nchini. Akizungumza Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, leo tarehe 30 Aprili 2025 baada ya kuzindua Mashine za kisasa za kufagia barabara amewahimiza watendaji wa kampuni hiyo kutunza mashine hizo ili ziweze kuleta tija kwa shirika. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata, amefafanua uwepo wa Mashine hizo kutaiongezea kampuni hiyo uwezo zaidi…

  • Mkurugenzi SUMAJKT awataka Watendaji kutumia fursa

    Mkurugenzi SUMAJKT awataka Watendaji kutumia fursa. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata amewataka Wakurugenzi Waendeshaji, Wakuu wa Shule na Miradi kutumia vizuri fursa zilizopo katika maeneo yao ya kazi ili kuongeza tija kwa Shirika. Brigedia Jenerali Ngata ameyasema hayo tarehe 15 Agosti 2025 katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya SUMAJKT (KUS) kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Mlalakuwa jijini Dar es Salaam. Akizungumza katika kikao hicho Brigedia Jenerali Ngata amehimiza kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo ya Shirika. Aidha, amewasisitiza kuendelea kuzalisha Bidhaa na kutoa huduma katika…

  • Waziri wa Ulinzi Zimbabwe atembelea SUMAJKT

    Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Oppah Kashiri, amefanya ziara Makao Makuu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Mlalakuwa Dar es salaam. Katika Ziara hiyo Mhe. Waziri Kashiri, akiwa na Waziri wa Ulinzi na JKT wa Tanzania Dkt. Stergomena Tax, alipatiwa taarifa ya shirika na kutembelea kiwanda cha Taa cha SUMAJKT Skyzone Co Ltd. Kilichopo Mlalakuwa na kiwamda cha Maji ya Kunywa cha SUMAJKT Bottling Co Ltd. Kilichopo Mgulani JKT.

  • WAZIRI WA ULINZI NA JKT AZINDUA BODI MPYA YA SUMAJKT

    Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb) ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya SUMAJKT kuendeleza mambo mazuri yaliyoanzishwa na Bodi ya shirika hilo iliyomaliza muda wake kwa kuweka mbele Ubunifu, Mikakati pamoja na kuibua Miradi mipya ya kiuwekezaji. Mhe. Waziri Rhimo Nyansaho, amezungumza hayo leo tarehe 14 Januari 2026 baada ya kuzindua Bodi Mpya ya Ushauri ya SUMAJKT katika ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa Chamwino jijini Dodoma. Aidha, Mhe. waziri Nyansaho amewapongeza wajumbe wapya kwa kuteuliwa kwao na kutoa rai kwao kuendelea kusaidia SUMAJKT kusonga mbele na kufikia malengo…

  • Waziri wa Ulinzi Comoro atembelea SUMAJKT Makao Makuu

    Waziri wa Ulinzi ambaye pia ni Katibu wa Rais nchini Comoro Mhe. Yousoufa Mohamed Ali ametembelea Makao Makuu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) ikiwa ni Mwendelezo wa Mazungumzo ya kushirikiana katika biashara baina ya Shirika Hilo na Comoro. Mhe. Yousoufa akiwa ameongozana na Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania – Comoro Khalfan Saleh amepokelewa na Kanali Robert Kessy kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata Makao Makuu Mlalakuwa Jijini Dar es salaam. Ikumbukwe, ziara hiyo ya Mhe. Yousoufa Mohamed Ali imetokana na Makubaliano ya Awali ya kibiashara kati ya SUMAJKT na…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *