Habari na Matukio

  • Waziri wa Ulinzi Comoro atembelea SUMAJKT Makao Makuu

    Waziri wa Ulinzi ambaye pia ni Katibu wa Rais nchini Comoro Mhe. Yousoufa Mohamed Ali ametembelea Makao Makuu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) ikiwa ni Mwendelezo wa Mazungumzo ya kushirikiana katika biashara baina ya Shirika Hilo na Comoro. Mhe. Yousoufa akiwa ameongozana na Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania – Comoro Khalfan Saleh amepokelewa na Kanali Robert Kessy kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata Makao Makuu Mlalakuwa Jijini Dar es salaam. Ikumbukwe, ziara hiyo ya Mhe. Yousoufa Mohamed Ali imetokana na Makubaliano ya Awali ya kibiashara kati ya SUMAJKT na…

  • Mkuu wa JKT na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT amuaga Jenerali Musuguri

    Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT Meja Jenerali Rajabu Mabele, akitoa heshima za Mwisho kwa Mwili wa Marehemu Jenerali David Musuguri (Mstaafu) katika hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo Dar es salaam. Tukio la Kuaga Mwili wa Marehemu Jenerali David Musuguri (Mstaafu) aliyefariki Oktoba 29, 2024 limeongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango. Viongozi wengine waliohudhuria Tukio hilo ni Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete, Waziri wa Ulinzi Dkt. Stergomena Tax, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda, Maafisa Majenerali, Maafisa…

  • Shule ya Jitegemee JKT yatimiza miaka 50, Jenerali Mhona atia neno

    Mkuu wa Tawi la Mafunzo na Oparesheni Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania JWTZ Meja Jenerali Ibrahim Michael Muhona ameipongeza Shule ya Sekondari Jitegemee JKT kwa kutimiza Miaka 50 Tangu kuanzishwa kwake. Akizungumza katika Sherehe ya Maadhimisho hayo zilizoambatana na Harambee maalaumu ya kuchangia maboresho ya Shule hiyo Meja Jenerali Muhona amesema JWTZ linaunga mkono dhamira ya Mageuzi inayofanyika, huku akitoa wito kwa walimu kuhakikisha Shule inaendeleza viwango bora vya Ufahulu. Kilele cha maadhimisho ya Miaka 50 ya Jitegemee JKT kilifanyika tarehe 01 Novemba 2024 ukumbi wa Isamuhyo Mgulani JKT. CHANGIA ELIMU KWA MABORESHO YA MIUNDO MBINU1.NMB….236100419222.CRDB…01508929587003.LIPA….22426113 TIGO.4.LIPA….54359412 VODACOMMajina…

  • Nyumba 5000 zakamilika Msomera

    Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujemga Taifa SUMAJKT, Kupitia Kampuni ya Ujenzi ya @sumajktccl limekamilisha awamu ya Kwanza ya Mradi wa Nyumba 2500 katika Kijiji cha Msomera wilaya ya Handeni Mkoani Tanga. Akizungumza mara baada ya kutembelea eneo la Mradi huo Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata amesema ameridhishwa na kasi ya utekelezaji iliyotumika kukamilisha nyumba hizo. Taarifa zaidi tizama video hii hapa chini..

  • SUMAJKT yazindua gari kuongeza ufanisi shule ya Kawawa

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amezindua Gari aina ya TATA Marcopolo kwa ajili ya Matumizi ya Shule ya Awali na Msingi ya Kawawa iliyopo Wilaya ya Mafinga Mkoani Iringa. Akizungumza mara baada ya Uzinduzi huo Brigedia Jenerali Ngata ameutaka Uongozi wa Shule hiyo kutunza Vitendea kazi vinavyo nunuliwa ikiwemo gari hilo ili viweze kufanya kazi kwa Muda mrefu kwa manufaa ya Shule na Shirika kwa Ujumla. Akitoa taarifa fupi kabla ya Uzinduzi huo Mkuu wa Shule ya Kawawa Kanali Ernest Sikaponda amelishukuru shirika kwa kufanikisha Ununuzi wa gari…