|

Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi

Naibu Waziri Mambo ya Ndani Mhe. Daniel Sillo ayashauri mashirika ya Kijeshi ndani ya Nchi wanachama katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kutumia Sayansi na Teknolojia katika uzalizalishaji wa bidhaa zao.

Mhe. Sillo amesema hayo leo tarehe 25 Februari 2025 alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa Mashirika yanayo milikiwa na  Majeshi ya  nchi za  Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika katika hoteli ya Geraffe iliyopo jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri Mambo ya Ndani ayashauri mashirika ya Kijeshi, Amefafanua kuwa Mkutano huo hufanyika kila mwaka ili kutathmini utendaji kazi wa Mashirika na Viwanda vilivyopo ndani ya Majeshi yaliyopo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ajili ya kubadilishana uzoefu.

Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zilizoshiriki mkutano huo ni nchi mwenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Jamhuri ya Demokrasia Congo, Sudan Kusini na Somalia.

Pamoja na kikao hicho wajumbe wa kikao kesho watatembelea Kiwanda cha Taa cha SUMAJKT Skyzon Co. Limited na maonesho ya bidhaa zinazozalishwa na mashirika ya Jeshi nchini Tanzania katika viwanja vya Golf Club Dar es Salaam.

Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube

Similar Posts

  • MKUU WA JKT AMSHUKURU RAIS NA AMIRI JESHI MKUU MAFUNZO YA JKT

    Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa Meja Jenerali Rajabu Mabele, ameishukuru Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleza mafunzo ya vijana wa JKT. Mkuu wa JKT amshukuru Rais na Amiri Jeshi Mkuu mafunzo ya JKT. Meja Jenerali Mabele, ameyasema hayo leo tarehe 17 Aprili 2025 alipokuwa anahitimisha mafunzo ya Awali ya kijeshi kwa vijana wa Operesheni miaka 60 ya Muungano katika kikosi Cha Ruvu JKT kilichopo mlandizi mkoani Pwani. Amesema Malezi ni suala Mtambuka, yanaanzia ngazi ya familia, Vijana wanapofika makambini….

  • SUMAJKT yazindua gari kuongeza ufanisi shule ya Kawawa

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata, amezindua Gari aina ya TATA Marcopolo kwa ajili ya Matumizi ya Shule ya Awali na Msingi ya Kawawa iliyopo Wilaya ya Mafinga Mkoani Iringa. Akizungumza mara baada ya Uzinduzi huo Brigedia Jenerali Ngata ameutaka Uongozi wa Shule hiyo kutunza Vitendea kazi vinavyo nunuliwa ikiwemo gari hilo ili viweze kufanya kazi kwa Muda mrefu kwa manufaa ya Shule na Shirika kwa Ujumla. Akitoa taarifa fupi kabla ya Uzinduzi huo Mkuu wa Shule ya Kawawa Kanali Ernest Sikaponda amelishukuru shirika kwa kufanikisha Ununuzi wa gari…

  • |

    RC CHALAMILA AAGIZA HALMASHAURI ZIFUNGE TAA ZA SUMAJKT

    Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Albert Chalamila ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zilizopo Dar es Salaam kuhakikisha wanafika kiwanda cha SUMAJKT Skyzone kilichopo Mlalakua jijini hapo ili kutoa oda za kutengeneza taa bora za barabarani. “Tumepita tumeona teknolojia ya kiwanda hiki., naomba nitoe neno rasmi.., wakurugenzi wote wa halmashauri za Dar es Salaam, kufanya ziara mara moja katika kiwanda hiki, na ikiwezekana kutoa oda za taa.., ili ziweze kufungwa kwenye mji wetu kuhakikisha mji unafanya kazi masaa 24.” Naye Mkurugenzi Mtendaji wa SUMAJKT Brigedia Jenerali Petro Ngata amesema kwamba Kiwanda hiko ni cha kwanza kabisa kwa aina…

  • |

    KAMISHNA WA JKT KUTOKA NCHINI NAMIBIA ATEMBELEA MAKAO MAKUU YA SUMAJKT

    Kamishna wa Jeshi la Kujenga Taifa nchini Namibia Dkt. Felix Masukubili amefanya ziara ya kikazi Makao Makuu ya Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), Leo tarehe 18 Novemba 2024 Mlalakuwa Jijini Dar es Salaam. Dkt. Masukubili amepokelewa na Mwakilishi wa Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa na Afisa Mtendaji Mkuu wa SUMAJKT ambaye ni Mkuu wa Chuo cha Uongozi JKT Kimbiji Kanali Festus Mang’wela. Akiwa katika ziara hiyo amejionea shughuli za uzalishaji Mali zinazofanywa na SUMAJKT ikiwemo kiwanda cha kutengeneza Taa cha SUMAJKT SKYZONE CO.LTD ambacho kinazalisha taa zinazotumia nishati ya jua na umeme, kilichopo Mlalakuwa…

  • |

    BRIGEDIA JENERALI NGATA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAFANYABIASHARA NCHINI COMORO

    Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi ka Kujenga Taifa (SUMAJKT) Brigedia Jenerali Petro Ngata amefanya mazungumzo na Jumuiya ya wafanyabiashara kisiwani Comoro katika ukumbi wa Chambre de Commerce Ngazidja uliopo kisiwani humo. Kikao hicho kimefanyika tarehe 5 Septemba 2024, na wafanyabiashara wanaochukua bidhaa Tanzania na kuzipeleka nchini Comoro, Brigedia Jenerali Ngata alipata fursa ya kueleza shughuli mbalimbali zinazofanywa na SUMAJKT hususani katika Sekta ya Ujenzi, Kilimo, Mifugo na Uvuvi. Aidha, Brigedia Jenerali Ngata ameeleza nia thabiti ya SUMAJKT kuhitaji kufanya kazi na wafanyabiashara hao katika nyanja ya Ujenzi na Kilimo. Kwa upande wa wafanyabiashara kisiwani Comoro wamesema…

  • RUVU JKT WAACHANA NA MATUMIZI YA KUNI NA MKAA

    Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax ameupongeza uongozi wa kikosi cha Ruvu JKT kilichopo Mkoani Pwani kwa kuachana na matumizi ya nishati ya kuni na mkaa na kuanza kutumia nishati ya gesi kwa asilimia 100. Ruvu JKT waachana na matumizi ya kuni na mkaa. Mhe.Dkt. Tax ametoa pongezi hizo tarehe 3 Aprili 2025 wakati alipofanya ziara kikosini hapo na kujionea namna kikosi hicho chini ya Uongozi wa kamanda kikosi Kanali Peter Mnyani unavyotekeleza kwa vitendo maelekezo ya serikali ya kuachana na matumizi ya kuni na mkaa kwa Taasisi zinazohudumia watu zaidi ya 100. Amepongeza ubunifu wa…

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *