Brigedia Jenerali Petro Ngata Ameitaka Kampuni ya Umeme ya SUMAJKT Electric  Co Ltd  kuvitunza vitendea kazi

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi la Kujenga Taifa (SUMAJKT), Brigedia Jenerali Petro Ngata Ameitaka Kampuni ya Umeme ya SUMAJKT Electric  Co Ltd  kuvitunza vitendea kazi vinavyonunuliwa  ili viweze kudumu na kuleta tija kwa Shirika.

Amezungumza hayo Tarehe 14 Februari 2025, baada ya  kufanya Uzinduzi wa Gari Jipya la utawala lililonunuliwa na Kampuni hiyo kwa lengo la kuongeza ufanisi.

Awali akitoa taarifa  fupi ya ununuzi wa gari hilo Mkurugenzi Mwendeshaji wa SUMAJKT Electric Co Ltd. Meja James Mhame, amesema kuongezeka kwa gari hilo kutarahisisha utekelezaji wa majukumu yao.

SUMAJKT Electric Co.Ltd  Inajishughulisha na Kandarasi mbalimbali za Miundombinu ya Umeme wa njia ndogo na Kati pamoja na uwekaji Umeme katika Majengo binafsi, Taasisi za Umma na Mashirika.Brigedia Jenerali Petro Ngata Ameisisitiza Kampuni ya Umeme ya SUMAJKT Electric  Co Ltd  kuvitunza vitendea kazi hivyo.

Endelea kutufuatilia kupitia website yetu ya https://sumajkt.go.tz/ na mitandao yetu ya kijamii ya facebook, Instagram na Youtube

Similar Posts

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *