Karibu SUMAJKT Construction Co Ltd.

SUMAJKT CCL ni moja ya Kampuni Tanzu za Shirika la Uzalishaji Mal la Jeshi la Kujenga Taifa.
Kampuni hii inayojishughulisha na kazi za Ujenzi hapa nchini.

Mnamo, tarehe 24 Novemba 2018 Kampuni hii ilisajiliwa rasmi na BRELA kwa jina la SUMAJKT Construction Company Limited (SCCL).

Kazi zinazotekelezwa na Kampuni ya Ujenzi ya SUMAJKT (SUMAJKT Construction Company Limited)

a. Ujenzi wa Nyumba za Makazi, maofisi na biashara.
b. Ujenzi wa barabara na madaraja.
c. Ujenzi wa Mabwawa ya maji na miundombinu ya maji.
d. Kazi zote za Umeme katika Majengo.
e. Kazi za Uhandisi wa Mitambo.

Kampuni inatekeleza kazi za Ujenzi na Uhandisi kupitia kanda zake saba za Ujenzi ambazo ni:

  1. Kanda ya Mashariki (Dar es salaam, Pwani na Morogoro).
  2. Kanda ya Magharibi (Kigoma, Katavi na Tabora).
  3. Kanda ya Kati (Singida na Dodoma).
  4. Kanda ya Kusini (Mtwara, Lindi na Ruvuma).
  5. Kanda ya Kaskazini (Kilimanjaro, Tanga, Manyara na Arusha).
  6. Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe na Rukwa) na,
  7. Kanda ya Ziwa (Mwanza, Mara, Kagera, Shinyanga na Geita).

Fanya kazi nasi leo

Tembelea ofisi zetu au bofya kitufe hiki kupata mawasiliano yetu..